Quantcast
Channel: MO BLOG » INTERVIEWS
Viewing all 48 articles
Browse latest View live

MAHOJIANO NA MILLARD AYO SEHEMU YA PILI.

$
0
0

UNAJUA KWAMBA MILLARD AYO ALIWAHI KUTOLEWA KATIKA CHUMBA CHA MTIHANI KWA KUTOMALIZIA ADA? 

Kama tulivyokuahidi msomaji wa Mo blog ifuatayo ni sehemu ya pili ya mahojiano kati ya Mhariri wa Mo Blog Lemmy Hipolite na Mtangazaji maarufu Millard Ayo.

Mo Blog: Tunamsikia Millard Ayo lakini hatujui ni nani hasa.?

Millard Ayo: Milliard Ayo ni kijana wa miaka 26 aliyezaliwa tarehe 26 Januari mwaka 1986 ni kijana aliyezaliwa katika hospitali ya Mount Meru na ni mtoto wa kwanza kwenye familia ya watoto wanne.

Ninatoka katika familia ya Mzee Afrael Ayo al maarufu kama ‘Chalii’ pale Tengeru mkoani Arusha.

Mo Blog: Tupe siri ya mafanikio yako pamoja na umaarufu ulionao.?

Millard Ayo: Kiukweli moja kati ya vitu vinavyonifanya mimi nipate mafanikio, namshukuru Mungu kwa sababu kwanza situmii vitu vinavyowaangusha watu wengi kwenye kazi kama hizi; kwanza kabisa mimi sinywi pombe na sijawahi kunywa tangu nizaliwe; nadhani inanisaidia pia kwa sababu wakati wote akili inakuwa ‘fresh’.

Mo Blog: Kwa kifupi tuambie ilikuaje mara ya mwisho tumekusikia Radio One ghafla Clouds FM.?

Millard Ayo: Clouds Fm walivutiwa na kazi yangu, nadhani waliona uwezo wangu kupitia show ya ‘Milazo 101’ niliokuwa nikiifanya Radio One so alinipigia simu bosi wao nakumbuka ilikuwa ni siku ya Jumatano akaniambia tuonane.

Ukizingatia mimi nilikuwa na dream sana kufanya kazi ‘Clouds’ hata wakati naingia college ya Journalism nilikuwa na ndoto za kufanya kazi Clouds.

Mo Blog: Ayo tufafanulie kote ulikopita na hatimae hapa ulipo.?

Millard Ayo: Kiukweli nimefanya kazi TVZ Zanzibar, Wapo Radio -Dar es Salaam na ITV/Radio One kwa miaka mitatu; kote nilikuwa nafanyakazi na sisemi kwa nia mbaya, lakini Clouds ni Radio ambayo nilikuwa nimei’dream’ kuifanyika kazi kwenye maisha yangu.

Mo Blog: Zungumzia filamu za ki-bongo, kwa mtazamo wako tunaelekea wapi.?

Millard Ayo: Filamu za kitanzania zamani nilikuwa siangalii, lakini sasa hivi naangalia sana kwa sababu napenda kujifunza sana, mimi sikuzote napenda mtu ambaye anakubali kurekebishwa.

Filamu za kitanzania zina soko kubwa sana kwa watanzania, kwa sababu watanzania wanapenda vitu ambavyo wanavielewa; vitu ambavyo vina’happen’ kwenye maisha yao. Pia hakuna kitu kizuri kuwaona watu ambao unawafahamu wakiigiza inaleta uzalendo zaidi.

Mimi ningependa kuona waigizaji wa Tanzania wakitumia muda mwingi zaidi kujiandaa kwa ajili ya movie na waandaaji watumie fedha nyingi kutengeneza filamu ziwe na ubora unaostaili na naamini zitauza zaidi.

Mo Blog:  Tupe siri ya sauti yako..?

Millard Ayo: Mwenyezi Mungu ndio anajua, Mwenyezi Mungu ndio muweza wa yote na Mwenyezi Mungu ndio aliyopanga kila ninachokifanya kwenye hii dunia. Amepanga niumbike au kuzaliwa niwe hivi. Najua kupitia Mwenyezi Mungu haya yote yamewezekana. Sauti yangu sijaitengeneza ni sauti ambayo nimezaliwa nayo.

Mo blog: Katika siku za hivi karibu kuna suala lililochukua nafasi kubwa katika midomo ya watu, suala la Freemason haswa kwa watu maarufu kama wewe. Unazungumziaje?

Millard Ayo: Mimi Freemason siijui naisikia tu kwa watu kwa hiyo siwezi nikatolea ufafanuzi zaidi kwa sababu sina elimu nayo, sijawi kushudia vitu kama hivyo kwa hiyo nawaachia wanaofahamu. Kwa kweli siwezi ku-comment’ chochote.

Mo blog: MO BLOG ingependa uzungumzie maisha yako ya kimapenzi maana tumesikia mengi.!

Millard Ayo: Wakati mwingine unapokuwa ni mtu wa kufahamika vinaweza vikazushwa vitu vingi sana, na kuna taarifa nyingi sana kuhusiana na maisha yangu ya kimapenzi ambazo sio za kweli.

Kiufupi ni kwamba mimi nina ‘girlfriend’ niko nae huu ni mwaka wa tatu sasa na ni huyo peke yake.

Mo Blog: Kumezuka utamaduni wa watu mbali mbali kufungua ‘Blogs’ hebu zizungumzie kama unavyozijua.

Millard Ayo: Kiukweli mimi napenda sana, kwanza watu wanaojituma kwa nguvu zao wenyewe . kufunguliwa kwa blogs nyingi kila siku sioni kama ni kitu kibaya ni kitu kizuri sana, kwa sababu kila mtu ana ubunifu wake, kila mtu ana nguvu yake. Cha msingi ni kufanya kitu ambacho kinaendana na lengo la kufunguliwa kwa blog. Napenda sana kuona blogs mbalimbali.

Mo Blog: Umekuwa mtangazaji muda mrefu sasa nini hutokisahau radioni?

Millard Ayo: Katika maisha yangu mimi sababu ya utangazaji nimewahi kufanya vitu vingi kwenye radio lakini kuna shows tatu ambazo siwezi kuzisahau ambazo niliweka nguvu nyingi sana. ‘Vipaji Halisi’-Wapo Radio, ‘Milazo 101’-Radio One na ‘Amplifaya’-Clouds FM.

Amplifaya ndio ninayofanya sasa hivi na nimeahidi moyoni nitazidi kuweka nguvu kuifanya vizuri zaidi kuanzia mwanzo hadi mwisho moto utakuwa uleule. Hii show sio kwamba naifanya kwa kuwa ni kazi hapana na-enjoy kufanya na nafurahi kuwa Clouds FM. Namuomba Mungu anipe nguvu.

Mo Blog: Changamoto gani unakutana nazo katika kazi wewe kama Millard Ayo..?

Millard Ayo: Kuna changamoto nyingi sana lakini labda kubwa ni pale ambapo ninataka niwe wa kwanza kutoa habari yaani nitoe ‘exclusive’. Hii ndio changamoto inayonifanya nichelewe kulala, ndio maana ukifungua web site yangu unaweza kuona nimeweka stori ya tukio lililotokea labda saa nane usiku. Ina maana nilikuwa eneo latukio. Napenda sana kuwa wa kwanza kutoa habari ‘always’.

Mo Blog: Kama Millard lipi tukio la kukumbuka sana duniani.?

Millard Ayo: Tukio la kukumbuka sana kwangu ni siku nipotolewa katika chumba cha mtihani wa kumaliza katika Chuo cha Uandishi wa Habari. Nilitolewa kwa sababu sikuwa nimemalizia kulipa. Baba yangu kipindi hicho gari yake ilikuwa imevamiwa na majambazi akipeleka watu mnadani. Lilipigwa risasi kwa hiyo likawa liko gereji. Ile hela ya akiba akawa ameitumia yote ikaisha na bado gari halikupona.

Halafu mama yangu ni mwalimu akawa amewalipia ada wadogo zangu waliokuwa wasoma katika hizi shule za Medium akawa hana pesa kabisa, yaani kwenda shuleni nilikuwa natembea wakati nauli ni shilingi 150/- au 200/-. Natoka Ngarenaro mpaka Stadium kila siku asubuhi na jioni kurudi nyumbani hata hela ya kula mchana inakosekana.

Baada kushindikana kabisa kupatikana ada, mama yangu akajaribu kwenda kuongea na wale masekretari ili wamkubalie nifanye mtihani kwa sababu alikuwa akijuana nao kinamna, lakini ikashindikana kwa sababu walikuwa wameachiwa maagizo kuwa siwezi kufanya mtihani mpaka nimalize ada na ilikuwa imebaki 300,000/-.  Nikiamini mama atamaliza nao nikaingia katika chumba cha mtihani nikaanza kufanya baada ya kama dakika 10 au 12 hivi nikaja kutolewa tena nakumbuka ulikuwa ni mtihani wa ‘Video Shooting’.

Yaani nilipotolewa nikawa niko na mama analia mimi nalia nakumbuka nililia sana maana mtihani huo ulikuwa ndio-final, inamaana nisipofanya inabidi nisubiri tena mwakani.  Mama akaniambia anakwenda asipopajua popote Mungu atakapo muongoza akatafute hiyo ada, basi nikamsubiri pale chuo chini kuna-kimgahawa nikalia sana mpaka dada mmoja aliyekuja kunihudumia chai akaniuliza unalia nini?

Akanibembeleza sana lakini nikawa nalia tu nashindwa hata kuongea akaniambia hata hiyo chai kunywa tu bure usilipe sema unataka nini kingine mi nikawa nalia tu.

Baada ya kama dakika 35 au 45 hivi nikamuona mama anakuja ‘speed’ anakimbia akitokwa machozi akaniambia nimepata hela mwanangu twende. Tukapanda tena mpaka ofisi ya chuo akalipa mimi nikaambiwa niende kwenye chumba cha mtihani.

Nashukuru kwamba somo lenyewe nilifaulu nilipata 93 kwa sababu nilikuwa nalipenda. Yaani jambo hili ndugu zangu wana Mo Blog sitakisahau.

Mo Blog : Pole sa ndugu yetu kwa kisa kilichowahi kukuta lakini ndio mitihani ya maisha.

Mo Blog: Millard unafikiria au kutamani kufanya kazi na radio gani nyingine..?

Millard Ayo: Kwa sasa sifikirii kwenda redio nyingine mimi bado niko Clouds na Clouds ni familia yangu.

Mo Blog: Tunakushukuru kwa muda wako kuzungumza na MO BLOG na tunakutakia mafanikio mema katika kazi na Mungu akubariki.

Millard Ayo: Akhsante sana wadau wangu.


UNAMJUA MBUNIFU MAHIRI WA MAVAZI YA ASILI GABRIEL JOSEPH? AMEFANIKIWA KUJENGA MRADI WA MAJI UNAONUFAISHA ZAIDI YA WATU 4,000 KIJIJINI KWAKE..! SASA ANAMIKAKATI YA KUJENGA ZAHANATI KIJIJINI KWAKE.

$
0
0

Mbunifu wa Mavazi Gabriel Joseph (kushoto) akizungumza na Mhariri Mkuu wa MO BLOG Lemmy Hipolite.

KUPATA UNDANI WAKE FUATILIA MAHOJIANO YAKE ENDELEA KUPERUZI MO BLOG – USIKOSE…! !

EXCLUSIVE INTRERVIEW: MBUNIFU WA MAVAZI GABRIEL MOLLEL AASA KUWA WASIPOSHIRIKIANA WATAANGUSHA TASNIA YA UBUNIFU WA MAVAZI TANZANIA.

$
0
0

Mo Blog: Wewe ni mbunifu mwenye jina kubwa hapa nchini na nje ya nchi hii ulianza lini?

Grabriel Mollel: Mimi naitwa Grabriel Mollel ni mbunifu wa mavazi ninamiliki Kampuni inaitwa Sairiamu Design ambayo nimeanzisha kutoka mwaka 2009.

Mo Blog: Nini mafanikio yako tangu uingie kwenye fani hii ya ubinifu.?

Grabriel Mollel: Unajua mafanikio sio kuwa na hela benki ila unaangalia umetoka wapi na uliowakuta wamefanya nini na wewe umefika wapi..! Kwa sababu ni mwaka 2010 tu nilifanikiwa kuingia katika Maonesho ya Swahili Fashion ambayo kwangu nahesabu kama ni moja ya mafanikio yangu.

Mwaka 2011 nilifanikiwa kwenda Angola ambapo Swahili Fashion walinichagua tukiwa na Mustafa Hassanali, lakini vile vile Millen Magesse alitufanya sisi tukawa wageni maalum katika onesho la African Fashion Week la Afrika Kusini ambapo hapo nilijifunza mambo mengi sana.

2012 mwezi wa tatu nilifanikiwa kwenda Kampala ambapo mimi mwenyewe ndio nilikuwa ‘Main Designer’, kwa sababu ma-designer wengine walionyesha nguo 10 lakini mimi nilionyesha nguo 25, ikiwemo nguo moja wa ‘Ufukweni’ (Beach wear) ambapo kwa namna nilivyoibuni hapa Tanzania huwezi kuonyesha lakini Uganda unaweza ndio maana nikaenda kufanya ‘launch’ kule Kampala.

Pia sasa hivi nina ofisi tatu, mbili ziko eneo la Makumbusho, moja wapo ikiwa ni ofisi yangu binafsi, na nyingine inahusika na uzalishaji na bidhaa zangu wako watu ambao wanatembeza jioni na pia nina wateja wa nje.

Tangu 2003 nimekuwa nikimiliki ofisi ambayo iko Slipway japo ni gharama lakini siku zote ukitaka kupata fedha inabidi utumie fedha. Lakini ofisi yangu kwa pale inajulikana kama Masai Art Shop lakini iko chini ya Brand ya Sairiamu Designs.

Mo Blog: Unatengeneza bidhaa za aina gani na wateja wako wa nje uliwapataje.

Grabriel Mollel: Mini natengeneza mavazi na pia ‘Sandals’ na wateja wangu wa nje niliwapata kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook. Natengeneza na Vidani, herein na bangili za mikononi. Pia nakodisha nguo kwa sababu nguo zangu ninazobuni ni tofauti sana kwa sababu nime-base sana kwenye mambo ya asili. Ni nguo ambazo zinavaliwa katika shughuli muhimu muhimu sio ya kuva barabarani.

Mo Blog: Baada ya kupata mafanikio umeweza kuisaidia vipi jamiii ya watu ulikotoka?

Grabriel Mollel: Nilipopata mafanikio nikafikiria nilikotoka kuna ukame, nikafikiria mradi na nimefanikiwa kuleta maji kijijini  kwa kutumia marafiki niliokutana nao kutokana na kazi hii ninayoifanya.

Mradi huo kwa sasa unanufaisha watu 4,000 kijijini, na sasa hivi tunategemea kuwapeleka wasichana wawili hospitali ya Mbweni .  Wao watasoma kozi fupi na wakimaliza watarudi kijijini kusaidia kwa sababu kijijini kwetu hakuna hospitali nyingi wala wataalam.

Gharama hizo zinabebwa na Shirika Lisilo la Kiserikali lililopo chini yangu mimi kama Mwenyekiti na linaitwa ‘The Sairiamo Community Action Foundation’ ambayo nimeisajili mwezi wa pili na tunategemea ‘funds’ kutoka Italia.

Mo Blog: Nini matarajio ya Ngo yako baada ya wasichana hao kuhitimu?

Grabriel Mollel:  Baada ya kuwarudisha wale wasichana kijijini tuna mikakati ya kujenga zahanati kijijini. Kule hakuna zahanati karibu. Kwa sababu zamani wanawake walikuwa wanatembea kilometa 18 kupata maji, bado wanatembea kilometa 18 kufuata zahanati. Kwa vipi utamfikisha huyu mgonjwa hospitali?

Mo Blog: Tuzungumzie ‘bifu’ baina ya wabunifu zipo kweli na kama zipo nini tatizo?

Gabriel Mollel: Kusema kweli bifu zipo lakini kwa mimi naona ni kutokana na watu kuzidiana uwezo, pia kutaka kuzibiana riziki na pia kingine katika tasnia hii kuna unafiki.

Mo blog: Gabriel Joseph unaposema unafiki tufafanulie hapo.

Gabriel Mollel:  Ninamaanisha kwamba kuna watu wengine unafanyanao kazi na wanakuchekea lakini moyoni kwao hawako na wewe kabisa, na kwa sasa hali ni mbaya kwa sababu imengia na hata kwa ma-models.

Moja ya Ubunifu wa Gabriel Mollel.

Mo Blog: Kivipi?

Gabriel Mollel: Usipomchagua Fulani kuonyesha mavazi katika show yako itakuwa maneno, lakini kusema ukweli kama mimi naangalia aina ya nguo yangu niliobuni na je? Itafaa kuvaliwa na mwanamitindo mwenye umbo gani, sasa kama haeundani  na design yangu nifanyeje? Nikuchague tu ili nikufurahishe halafu mimi ni-fell katika kazi yangui?

Kingine pia waandishi hawako makini na kazi zao, wanaandika bila ya kuthibisha habari wanazoziandika, huwa zinachangia kutuvuruga wabunifu.

Mo Blog: Nini  Ushauri kwa wabunifu wenzako?

Gabriel Mollel: Kuna watu wanatishiana ubaya,  nawashauri sio kitu kizuri na pia tujenge utamaduni wa kusaidiana aliyeko juu amnyanyue anayechipukia.

Model na Vazi la Ubunifu wa Gabriel Mollel.

Mo Blog: Mbunifu gani wa mavazi hapa nchini ambaye kwako unampa ‘Big Up’ ?

Gabriel Mollel:  Kwa kweli namuamini sana Daiana Magesa, na Manju Msita namheshimu  kwa ubunifu wake.

Mo Blog: Tuambie umewahi kupata tuzo yeyote katika shughuli zako hizi za ubunifu wa mavazi?

Gabriel Mollel: Ndio nimewa kupata tuzo kama ifuatavyo:-

-The Most Innovative Designer of The year – 2011

-The Best Designer of the Year -2011

-The Men Wear of The Year -2011 –Swahili Fashion Week

-Red Carpet Designer of the year

Mo Blog: Kipi kimewahi kukukera katika shughuli zako hizi.

Gabriel Mollel: Kuna wakati Swahili Fashion week kulikuwa na mizengwe na ubabaishaji mwingi, mambo yalikwenda ndivyo sivyo lakini yote sawa nitaendelea na ubunifu wangu wa kutumia vitu vya asili.

Mo Blog: Neno la mwisho kwa tasnia ya ubunifu.

Gabriel Mollel:  Asanteni sana Mo Blog kwa kuja kuzungumza na mtu kama mimi naombeni muendelee kuwatembelea wabunifu wengine wa mavazi, kingine kwa wabunifu wenzangu tuwezeshane, tushirikiane na tushikamane ili kukuza fani hii, mwisho kabisa tusikatishane tamaa kwa sababu wako baadhi ya watu ukitaka kuanza ubunifu wanakukatisha tamaa na kukukandamiza chini.

Nawaambia hayo sio maadili ya ubunifu, ukiona mtu anajaribu msaidie.

Mo Blog:Gabriel Mollel sisi wana Mo Blog tunakutakia mafanikio mema na uweze kuzitangaza bidhaa zako za kiasili kwa wingi nje ya nchi kwani utakuwa umeitangaza Tanzania kwa ujumla.

Gabriel Mollel:  Akhsanteni sana nawakaribisha watanzania wote kuangalia bidhaa zangu katika maduka yangu na Mungu awabariki.

“I WILL REACH FAR; I KNOW WHAT I AM DOING BECAUSE I HAVE STARTED FROM SCRATCH.”

Mahojiano na: Lemmy Hipolte na Gabriel Joseph.

Picha na : Jofrey Mwakibete.

Msimamizi: Zainul Mzige.

 

TAZAMA VIDEO CLIP YA MAHOJIANO NA MHE. DR FAUSTINE NDUGULILE PART 1.

$
0
0

Sehemu ya kwanza kati ya mbili za mahojiano na Mbunge wa Kigamboni (CCM) Dr Faustine Ndugulile ambaye ameeleza mengi kuhusu kongamano kuu la UKIMWI alilohudhuria hapa Washington DC, hali ya mapambano ya UKIMWI nchini Tanzania na pia harakati zake BUNGENI.

Kagusia mgogoro wa MJI MPYA wa KIGAMBONI na mengineyo.

Karibuni

MSANII WA TANZANIA SAFINA DAUDI AWA MMOJA KATI YA WASANII 3 WALIOLIWAKILISHA BARA LA AFRIKA KATIKA TAMASHA NCHINI IRAN.

$
0
0

Msanii wa kitanzania mwanadada Safina Said Kimbukuta (wa kwanza kushoto) akiwa naa baadhi ya wasanii wenzake kutoka mataifa mbalimbali aliokutana nao Iran.

Msanii wa kitanzania mwanadada Safina Said Kimbukuta amepata bahati ya kwenda kushirikii Tamasha la Sanaa za uchoraji la kimataifa nchini Iran mnamo tarehe 4 September mwaka huu.

Tamasha la 19 la kimataifa la Sanaa la visual ambalo limefanyika katika mji wa Gorgan kaskazini mwa Iran, liliwashirikisha wasanii vijana kutoka mataifa mbalimbali, kukiwa na idadi ya washiriki kutoka nchi kumi na nane ulimwengu, ambalo lilianza tarehe 4 September mpaka 8 September 2012.

Aliporejea alipata wasaa ya kutembelea kituo cha utamaduni cha ubalozi wa Irani jijini Dar as salaam, ifuatayo ni mahojiano aliyoyafanya na jarida la Al-hikma:

Al-hikma: Hii ni Mara yako ya kwanza kutembelea Jamhuri ya Kiislam ya Iran, kiujumla imeichukuliaje safari yako na Taifa hilo la kiislam la Iran?

Safina Kimbukuta: Kwanza napenda kuchukua fursa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kwenda na kurudi salama, kwa kweli ni faraja na fakhari kwangu kupata fursa adhimu kama hii ya kutembelea nchi ya Jamhuri ya Kiislam ya Iran ni nchi nzuri yenye maendeleo makubwa katika safari yangu nimejifunza mambo mengi na kukutana na  watu kutoka tasnia mbalimbali, kama vile wasanii waandishi wa habari, walimu na wanasiasa.

Al-hikma: Wasanii kutoka Tanzania na Africa walikuwa wangapi na vipi yalikuwa maonyesho?

Safina Kimbukuta: Maonyesho yalikuwa mazuri yaliyokutanisha wasanii mbalimbali ulimwenguni, Kwa upande wa Tanzania nilikuwa Mimi peke yangu na Africa tulikuwa washiriki watatu, Tanzania, Senegal na Zimbabwe.

Al-hikma: Ni kitu gani ulichojifunza na kukuvutia katika Tamasha hilo?

Safina Kimbukuta: Kitu ambacho nilichojifunza na kunivutia ni jinsi ya ustadi wa kazi za wasanii wenzangu ambacho kabla ya hapo nilikuwa sijuwi lakini nashukuru kupitia tamasha lile nimejifunza mengi.

Al-hikma: je kuna kufanana Kwa Sanaa za kazi zako na washiriki wengine na aina ipi ya muundo ulikuwa ukitumia?

Safina Kimbukuta: Kazi za wasanii zilkuwa tofauti, Mimi binafsi nilitumia Metro Structure ambayo ni muundo tofauti na wasanii wengine.

 Al-hikma: Je washiriki wenzio waliichukuliaje kazi za Sanaa yako?

Safina Kimbukuta: wameipokea vizuri kazi yangu japokuwa sikuweza kuzimalizia kutokana na mda kuwa finyu lakini wasanii wenzangu wameonyesha kuvutiwa na kazi zangu.

Al-hikma: Je watanzani wakipata fursa Kama hii unadhani wana weza kuonyesha ushindani wa aina yoyote?

Safina Kimbukuta: Nafikiri watanzania wanao uwezo wakipata fursa kama hizi kushiriki na kuonyesha ustadi wa kazi zao kwa jamii nyingine.

Al-hikma: Umeichukukulisje Iran katakona na mtazamo wa propaganda wa nchi za kimagharibi?

Safina Kimbukuta: Kwanza nilipopata habari juu ya ushiriki wangu wa tamasha la Sanaa nchini Iran, ndugu zangu walishangaa Sana na kuniuliza maswali mengi iweje Iran? Isiwe nchi nyingine, lakini nilivyofika na kukaa mda wa siku tano, mambo Leo yanayozungumzwa na vyombo vya magharibi ni tofauti kabisa na hali halisi iliyopo Iran ni nchi yenye wananchi wenye upendo na amani na nawashauri watanzania wenzangu na kuwaambia kuwa Jamhuri ya Kiislam ya nchi ni yenye ustaarabu  uhuru kamili kwa jamii yoyote na napenda kuwashukuru Kituo cha Utamaduni cha Ubalozi wa Kiislam wa Iran nchini kwa kufanikisha safari yangu na kurudi salama. 

SHIBUDA AWATAKA WANASIASA KUEPUKANA NA MDUDU SHETANI WA KUJINUFAISHA WENYEWE.

$
0
0

Mo Blog: Shibuda umekuwa mwasiasa kwa siku nyingi nini rai yako kwa viongozi wenzio wa kiasiasa.?

Shibuda: Napenda kutoa rai kwa vyama na viongozi wa kisiasa ambavyo viko karibu 21 hapa Tanzania, la kwanza kila chama kijifanyie tathmini, kinawajibika vipi kutekeleza mipango ya kuendeleza amani na utulivu katika hii nchi.

Vinatekeleza mipango gani? Na kila chama kifanye tathmini kijiuze mambo gani ambayo ni makosa kwa ustawi na maendeleo ya nchi yetu inaoongozwa na kulindwa na tabia, mila na desturi za mtanzania.

Vyama vya siasa viwe na wito unaoitwa ‘kwa maslahi ya umma’ na viongozi pia watekeleze wito unaoitwa kwa maslahi ya umma.

Mo Blog: Kwani una shaka na baadhi ya vyama?

Shibuda:Vyama ambavyo vina mdudu shetani anayeitwa ibilisi wa kujenga tafrani, migongano, misuguano au vyama vinavyoitwa ‘chama kampuni’ kwa maslahi binafsi, havistahiki kuwa sehemu moja wapo ya mbegu ya kuzalisha amani.

Hivyo watanzania tutafakari, tusemezane, tutazame viwango vya kila chama, katika vyama 21 kwamba je? Tija ya kila chama ni kwa kujenga ustawi na maendeleokwa jamii? Ili mwaka kesho tusherehekee tena siku ya amani duniani.

Mo Blog: Lipi la msingi ungependa kusisitiza kwa watanzania?

Shibuda: Jambo la msingi ningependa kusisitiza ni kwamba watanzania tuanze kupambanua, tuanze kutafakari, tuanze kusemezana kuwa hivi vyama 21 ni mapumulio dhidi ya majinamizi na dhuluma ambazo taifa hili limekuwa nazo kwa muda mrefu dhidi ya ustawi wa jamii?

Mimi ningependa kusisitiza ya kwamba watanzania wenzangu tupokee vyama 21 kuwa ni changamoto ya mchakato wa kuwa tuna sauti ya umma, yenye mti mmoja wenye mchipuo unaoitwa uzalendo, uaminifu na utiifu kwa maslahi ya umma.

Matawi haya 21 yaonekane kweli yanawakilisha maslahi ya umma.

Mo Blog: Lakini kwani una shaka na lipi au na nani?

Shibuda: Lakini kama kuna watu wamejiona tu ya kwamba wana mashinikizo na matatizo yao binafsi wakasema kwamba tunaanzisha chama, wajue kuwa hiyo ni SACCOS ambayo haina ustawi na maendeleo ya nchi bali wanatafuta michango, wanatafuta wapate ruzuku wapate kuchangiwa kwa maslahi yao binafsi.

Chama lazima kitambulishe juhudi zake, jitihada zake, dhamira, azma ya kuhakikisha ya kwamba wana wito wa kuwatumikia watanzania kwa ari moja, nguvu mpya na kuhakikisha kweli ni uamsho kwa ustawi na maendeleo ya Tanzania.

Mo Blog: Kwani unashaka kuwa nini kitatokea yasipofanyika hayo unayoyasema?

Shibuda: Ninachokisema ni kwamba la si hivyo tutakuwa na vyama vingi ambavyo ni sawasawa na nyumba ambayo ina bati moja lakini limetoboka toboka na linaingiza mifereji ya maji ndani ya nyumba, badala ya kupata sakafu iliyokavu, tunajikuta tunahamisha vitanda kupeleka huku na kule lakini kila unakopeleka kitanda chako kunavuja, hatutaki watanzania imani zao ziwe za kutangatanga.

Mo Blog: Kwa kumalizizia lipi neno unaachia watanzania?

Shibuda: Kila mtanzania apate mgutuko anapoona viongozi wa chama hawana maadili mema, hawana wito, hawana vitendo, hawana kauli zinazoshabihiana na mtu mwenye wito wa kutumikia au kama shekhe ama askofu hana vitendo vinavyoshabihiana na imani yake, basi ujue huyo ni mtu tu sawa na chui aliyevaa ngozi ya kondoo ili aingie kwenye zizi lakini dhamira yake ni kuwatafuna.

Tujitahadhari na watu ambao wamekuja na jina la siasa lakini kumbe ni chui mla watu.

Mahojiano na Picha: Lemmy Hipolite na Jofrey Mwakibete.

Msimamizi: Zainul Mzige.

 

TEJA ALIYEIBUKA KUWA MWANA SANAA AONGEA NA MO BLOG NA KUWAAMBIA VIJANA KUBWIA ‘UNGA’ NI KUCHUNGULIA KABURI.

$
0
0

*MATEJA WAAMBIWA WACHAGUE MOJA KATI YA KIFO AU KUACHA MADAWA YA KULEVYA*

 MO BLOG: Tupe histioria fupi ya maisha yako..!

MWIRU: Naitwa Zakaria Antony Mwiru nikiwa mzaliwa wa Kusini mwa Tanzania lakini wazazi wangu walihamia Dar es Salaam nikiwa na umri wa miaka 2, hivyo nimekulia Dar es Salaam na kusoma Shule ya Msingi Kinondoni A na Nikasoma Shule ya Sekondari Kinondoni Muslim mpaka Kidato cha 4 bahati mbaya nilifeli hivyo nikajiunga na Chuo cha Sanaa Bagamoyo kwa muda wa miaka 3 nikasoma sanaa za ‘Wood Carvings’, ‘Sculpture’, ‘Painting’ na ‘Ngoma za Utamaduni’.

Baada ya kuhitimu kwa miaka mitatu nilifanya shughuli zangu za sanaa kwa muda wa kama miaka mitano hivi, na baadae nikajikuta nimeingia katika sakata la dawa za kulevya.

MO BLOG:  Badala ya kuendelea na sanaa uliyojifunza Bagamoyo ilikuaje ukaingia katika mkumbo wa matumizi ya dawa za kulevya.

MWIRU: Nahisi sababu iliyonipelekea kuingia kwenye mkumbo wa dawa za kulevya ni kutohisi kuwa na furaha kwa maisha ninayoishi na nikategemea kwamba nitapata furaha zaidi kama nitatumia ulevi, kwa hiyo nikaanza na bangi kisha pombe  na baadae nikaingia katika matumizi ya Heroin.

Lakini vile vile sikupata ile furaha niliyokuwa naitegemea na matokeo yakawa mabaya zaidi na baada ya muda mrefu nilichoshwa na ile hali iliyojaa mateso ndani yake.

MO BLOG: Umetumia dawa za kulevya kwa takriban miaka mingapi?

MWIRU: Nimetumia dawa za kulevya kwa takriban miaka 10, yaani ukichanganya tangu nianze kutumia pombe, bangi na unga, lakini hapo mwanzo nilitumia kama miaka minne kwenye bangi na pombe na miaka sita nikatumia na Heroin.

 MO BLOG: Unaweza ukatuelezea umepata madhara gani baada ya kutumia madawa hayo.?

MWIRU: Ndio; unajua kwenye hii program yetu tunasema ‘Siri Zetu Ndio Madhara Yetu’ sasa mimi dawa za kulevya zilinisababisha nikapata Hepatitis B. Hii ni homa ya ini lakini ambayo inaweza kutibika ambapo ningepata Hepatitis C ini lingekuwa limearibika kabisa. Niliambiwa kama ningeendelea kutumia ningepata Hepatitis C.  

Madhara mengine niliyopata japo sio makubwa sana nilipoteza uhusiano na ndugu zangu na familia yangu, nikapoteza uaminifu kwa watu wangu wa karibu vitu ambavyo viliniumiza sana.

MO BLOG: Uliijuaje na ilikuaje ukaingia ‘SOBER HOUSE’..?

MWIRU: Mara ya kwanza niliisikia ‘SOBER HOUSE’ lakini sikuweza kuingia. Lakini bahati nzuri nilikuwa na rafiki yangu alikuwa ni raia wa Sweden, alikuwa ananipenda na nilifanya nae biashara sana na kazi zangu alikuwa ana nunua mara kwa mara na alivutiwa nazo sana.

Siku moja aliniita akaniambia kuna swali anataka kuniuliza nika mwambia niulize tu! Akaniambia nimwambie ukweli kama natumia Heroine au situmii. Kwa hiyo mimi siku hiyo nikaona siwezi kufanya tena siri, kwa sababu siku zote alikuwa rafiki yangu lakini nilikuwa nimemficha.

Siku hiyo nikaamua nikakiri mbele yake kwamba natumia Heroin, baada ya kukiri akaniambia ananipenda sana na yuko tayari kunisaidia kuachana na matumizi ya Heroin. Akasema ni bora uvute bangi au unywe pombe kuliko kutumia Heroine. Akasema atanisaidia kuacha lakini itanikosti; nikakubali nikamwambia nitalipia hizo gharama.

Yeye ndiye aliyenipeleka ‘SOBER HOUSE’ akanilipia miezi mitatu akatoa kitu kama laki tano kwa ajili ya ada yangu na nyingine za matumizi yangu nitakapokuwa humu ndani. Hivyo sio uwezo wangu mimi lakini Mwenyezi Mungu alinichagua kwamba huyu mtu nataka nimuokoe lakini kupitia kwa mtu.

Na alikuwa ni mtu si wa kutoka kwenye familia yangu kwa sababu hata wazazi wangu nilikuwa naogopa hata kuwaambia natumia Heroin kwa sababu sikuona kama ni sifa nzuri. nisingeweza kwenda kuwaambia wanipeleke ‘SOBER HOUSE’ hivyo Mungu akanitumia mtu akanisaidia na mimi nikapokea ule msaada na mpaka sasa situmii tena madawa hayo. Na Yule m-Sweden aliniambia shukran nitakayompa ni kutotumia tena Heroine.

Msanii Zakaria Mwiru akionyesha sanamu ya Bi. Kidude kwenye maonyesho yaliyofanyika hivi karibuni.

MO BLOG: Yapi unaweza kuyataja kama mafanikio baada ya kuacha kutumia Heroin.?

MWIRU: Mafanikio ambayo naweza kuyataja baada ya kipindi hichi cha mwaka mmoja na miezi kadhaa tangu kuacha kutumia dawa, kwanza ninaweza nikafanya kazi bila kutumia kilevi, naweza kula chakula bila kutumia stimu na naweza kupata usingizi bila kutumia dawa kwangu ni mafanikio tosha, kwani mwanzo nilikuwa siwezi.

Kingine kwa sasa naweza kumiliki vitu vya material, kama simu, kompyuta, ipad na vingine kwa sababu zamani nilikuwa siwezi kuvimiliki nikivipata nawaza kuviuza ili nikapate dawa za kulevya.

MO BLOG: Vijana ambao bado mpaka sasa wanatumia madawa ya kulevya unawaambia nini.?

MWIRU:  Kwa sababu mimi mwenyewe nilitumia madawa ya kulevya kwa kipindi kirefu, nikajaribu kuacha nikashindwa na nilishindwa kwa sababu ya yale maumivu unayoyapata unapoacha, ningependa kuwaambia vijana wenzangu wavumilie hayo maumivi ya saa 72 tu kama siku tatu tu. Kama unavyojua ‘No Gain Without Pain’ kwa vijana nawaambia kuwa mwenyewe kuacha ni ngumu sana lakini tukiwa pamoja tukashirikiana inawezekana.

MO BLOG: Kuna kundi la vijana ambao hawajawahi kutumia dawa za kulevya , hawajui stimu yake, hawajui maumivu yake wala madhara yake, hawa unawaambia nini.?

MWIRU:  Vijana hawa nawahusia wasije wakasema najaribu nione raha yake itakaa vipi, kwa sababu hata mimi mwanzo nilijaribu nikaona kama nzuri mwisho wake ukawa mbaya. Nawahusia vijana wenzangu ambao hawajawahi kushika dawa wasianze; kwani wakigusa mara ya kwanza tu watakuwa wameingia kwenye maradhi ya uteja. Kikubwa wasiwe na tama ya kufanya mambo ya kuiga.

MO BLOG: Swali la kizushi vipi mahusiano yako na wanawake wakati unatumia dawa za kulevya.?

MWIRU: Kwanza nilikuwa na mahusiano mazuri na wanawake lakini nilipoanza kubwia mwanamke wangu alikuwa unga.

Kwa mfano mimi ni mwanasanaa hivyo katika biashara yangu walikuwa wakija wanawake kibao hasa wa kizungu wakifurahishwa na kazi zangu wengine walitaka mahusiano lakini sikuwa na dili nao nikuwa nawaza unga tu.

Nilikuwa nafanya nao biashara kwa ajili ya kupata hela, lakini niliwaambia sitaki kwenda Ulaya walanini.
Mimi ilikuwa badala nijenge daraja la kukutana na watu wazuri nilikuwa najenga ukuta naishi maisha ya kujitenga na kuishi maisha ya ubinafsi.

Pete aliyokabidhiwa na mama yake mzazi kama zawadi baada ya kuacha kutumia madawa ya kulevya.

MO BLOG: Baada ya kuacha kutumia dawa za kulevya mahusiano yako na familia yakoje?

MWIRU:  Uhusiano wangu na familia mpaka sasa hivi naweza kusema umekaa vizuri, kwa sababu baada ya kuacha dawa hizi nilikwenda kwa mama yangu na akanikumbatia kwa mara ya kwanza ikiwa imepita zaidi ya miaka 10 hajawahi kunikumbatia. Na akanionyesha upendo na kunizawadia pete akaniambia hii pete yako ya Baraka. Akaniambia kuwa na kama utataka tena kuvuta madawa hii pete yangu nirejeshee.

MO BLOG: Kwa kifupi tuambie kuhusu haya maonyesho ya SOBER HOUSE na utaratibu mzima na pengine mtu anataka kujiunga lakini hana uwezo.?

MWIRU: Kuna utaratibu mzuri umeandaliwa kwa sababu mtu anapotaka kujiunga sio lazima alipe kwa mkupuo, anaweza akalipa awamu ya kwanza kwa malipo ya dawa zake za maumivu anapokuwa ndani ya nyumba halafu, nyingine ni kwa ajili ya matumizi yake kama maji, kulala, umeme n.k.

Na wakati huohuo anashiriki masomo.

MO BLOG: Je waonaje hicho kiwango mnacholipia, mtu wa kawaida anayetumia dawa za kulevya kama mpiga debe anaweza kukimudu?

MWIRU: Kwa kweli kama ndio umeshaanza kutumia na kufukuzwa nyumbani kiwango hicho ni kikubwa, lakini mtu huyu anahitaji msaada kwa wasamaria wema kwa sababu ukiangalia tu kula yake kwa siku inazidi 3000. Naweza kusema.

MO BLOG: Kwa uzoefu wako unadhani nini hasa kinacho wapelekea vijana kukimbilia kwenye utumiaji wa madawa ya kulevya.

MWIRU: Vijana wanakimbilia kwenye matumizi ya dawa za kulevya kwanza hawajui tatizo lake ni nini? Nadhani wengi wanakosa furaha na kudhani furaha wataipata kwenye matumizi hayo; cha msingi elimu inapaswa kuenezwa kwa vijana sio tu kukabili dawa za kulevya ila pia kubadili mwenendo mzima wa maisha haswa kufundishwa ustahimili.

MO BLOG: Kwa kumalizia Bw. Mwiru nini ushauri wako kwa watanzania kwa ujumla, kwa maana ya serikali, taasisi, wizara, vijana watumiaji na wasiotumia.

MWIRU: Kwanza kwa vijana wanaotumia wajaribu kutafuta wadhamini au wakiweza warudi kwa familia zao waombe kusaidiwa kwa sababu peko huwezi. Na kujikubali kwamba wana matatizo ya kutumia dawa.

Naiomba jamii isiwanyanyapae watu wanaotumia dawa za kulevya na kuwaona kama hawafai bali ichukulie kuwa ni njia moja mtu ameteleza na mtu huyo huyo kama atanyanyuliwa akatembea tena kwa miguu yake.

Kwa serikali natoa wito kutoa misaada katika hizi nyumba za kusaidia watu walioathirika na dawa za kulevya kama ilivyo ‘SOBER HOUSE’ ili ziweze kuwaelimisha vijana kutotumia dawa za kulevya.

Kwa sababu hatutaweza kuzuia watu wasiingize dawa za kulevya kwa sababu hata mataifa makubwa duniani yameshindwa kuzuia kwa hivyo msingi ni kuwaelimisha kutotumia, naamini watu wetu wakielimika soko la dawa hizo litazidi kupungua.

MO BLOG:  Nini kilikupelekea mpaka ukachonga sanamu ya Bi. Kidude? Na sio mtu mwingine maarufu Tanzania.

MWIRU: Ahh unajua nilipoingia Zanzibar mara ya kwanza nilimsikia Bi. Kidude kupitia filamu moja inaitwa maangamizi. Ilikuwa inazungumzia watu waliokuwa wanadharau wahenga na mambo ya kale. Nilivutiwa nayo sana kwa sababu huyu bibi nilimuona ni mwanamke anayeweza kusimamia utamaduni wa kiafrika.

Bi. Kidude namfananisha kama balozi wa Zanzibar anayewakilisha utamaduni wa Zanzibar kimataifa.Ndio maana nikavutiwa kutengeneza sanamu yake kwa sababu ameweza kustiki katika performing act tangu awali na mpaka sasa.

MO BLOG: Nani mwingine maarufu unafikiria kuchonga sanamu yake.?

MWIRU:  Baada ya hapa nafikiria kuchonga sanamu ya sura ya kila kiongozi aliyepita katika nchi hii.

MO BLOG: Haya ndugu yetu hapa Kassim Rashid jitambulishe wa wadau wa Mo Blog.

Baada ya kufahamu mengi kuhusu Zakaria Mwiru Mo Blog ilizungumza na meneja wa Sober House.

RASHID KASSIM:  Mimi ndie meneja wa nyumba inayoshughulika na kufanya ‘exhibition’ hii. Hii nyumba inaitwa ‘Sober House’ ambayo ipo maeneo ya Mpendae Zanzibar.

MO BLOG: Vikwazo gani unakabiliana navyo kuendesha nyumba hii ukizingatia unadili na watu waliokuwa tayari wamepinda kwa madawa?

RASHID KASSIM:  Vikwazo ni vingi kwa kweli ikiwemo malipo ya hawa watu wanaoletwa ndani ya nyumba. Kwa sababu sio muda wote wanafanya malipo kwa wakati muafaka nah ii inatupa ugumu sana inabidi watu kutoa fedha mifukoni mwao kwa ajili ya kuendesha nyumba hii.

Kikwazo kingine ni kama unavyojua watu waliomo humu ni wenye tabia tofauti hivyo inabidi kuwa na ustahimilivu na busara ili kuweza ku-‘deal’ nao.

MO BLOG: Wewe mwenyewe umewahi kutumia kama ndi kwa muda gani na ilikuaje ukaacha.

RASHID KASSIM: Ndio mimi nimetumia si chini ya miaka 15. Ilifika kipindi nikawa na machaguo mawili tu ama nife au niache tumia madawa. Kwa katika machagua hayo lililokuwa bora kwa niliona bora niache kuliko kufa. Kwa sasababu hata ningekufa bado tatizo lilikuwa nakufa katika kifo cha aina gani.

MO BLOG: Kwa ufupi tuelezee mafanikio baada ya kuanzisha nyumba hii.

RASHID KASSIM: Kwa kweli mafanikio ni mengi sana maana nyumba yetu hii ndio imezaa nyumba nyingine hizi zilizopo sasa za kuwasaidiwa watu wanaotumia dawa za kulevya.

Kingine ni kwamba tumepiga hatua kutoka katika ‘Recover’ tumekuja katika Sanaa. Japo mimi mwenyewe sifanya sanaa ila ndio msimamizi wa hawa wenzangu.

MO BLOG: Tunawashukuru sana Meneja Rashid Kassim Na Msanii Zakaria Mwiru kwa jitihada zenu katika kupambana na wimbi la matumizi ya dawa za kulevya na pia kuendeleza sanaa hapa nchini.

RASHID KASSIM NA ZAKARIA MWIRU: Akhsanteni sana Bwana Lemmy na Zainul tunaomba muendelee kutungaza hivi na blogs nyingine ziige mfano wenu ili vijana ambao bado wanatumia wajue bado wana nafasi ya kuacha na kujiendeleza.

 Zakaria Mwiru akiwa na na Meneja wa SOBER HOUSE Zanzibar Bw. Rashid Kassim.

Zakaria Mwiru akishow love na Assistant Operation Manager wa Mo Blog Zainul Mzige.

Mahojiano: Lemmy Hipolite – Chief Editor Mo Blog.
Msimamizi: Zainul Mzige – Assistance Operation Manager Mo Blog.

Kutana na Nusra Maguluko (28) Mwanamke Jasiri anayeendesha Basi La Shabiby, Dar-Dom.

$
0
0

Nusra akiwa kazini katika basi la Shabiby.

 *Ana ndoto za kufungua Chuo cha mafunzo ya udereva kwa wanawake ili waweze kuendesha magari makubwa.

*Basi lake hugombaniwa na abiria popote anapopakia, hujaza kwanza na kuondoka kisha mabasi mengine.

Na. www.sufianimafoto.blogspot.com

Nusra Maguluko (28) ni msichana jasiri na anayependa kujaribu na kupata mafanikio ya majaribio yake bila woga wala kujali ni aina gani ya kazi anayotakiwa kufanya yeye kama mwanamke na ipi asiyostahili kufanya yeye kama mwanamke.

Ni ujasiri wake hasa ndiyo ulimuwezesha kumfikisha hatua aliyonayo kwa sasa, ambaye ni miongoni mwa wanawake wachache na hasa kwa Tanzania waliopata kuifikia na kujiamini hadi kuwa na ujasiri wa kubeba roho za watu zisizopungua 40 kila safari moja ya kwenda Dodoma ama kotoka Dodoma kuja Dar.

Nusra ni mzaliwa wa Mkoa wa Manyara katika wilaya ya Kiketo, na ni mtoto wa nne kuzaliwa kati ya 12 wa familia ya baba yake mzazi mzee, Maguluko na Elimu yake ni Kidato cha pili tu.

Alimaliza elimu ya Msingi mwaka 1997, katika Shule ya Msingi Matui iliyoko Wilayani Kiteto, baada ya kuhitimu elimu ya msingi alijiunga na elimu ya Sekondari ambayo kwa bahati mbaya hakuweza kumaliza na kuishia Kidato cha pili baada ya kusumbuliwa na maumivu ya kichwa mara kwa mara.

Basi analoendesha Nusra likiwa safarini kuelekea Dodoma.

Nusra, alishauriwa na madaktari kupumzika kwa muda wa miaka mitatu bila kusoma ama kuwa akiangalia karatasi nyeupe mara kwa mara, jambo ambalo lilimfanya kuamua kumsumbua Baba yake mkubwa, Hamis Mang’endi aliyekuwa ni fundi wa magari ili amfundishe ufundi na udereva wa gari.

Baada ya kumsumbua sana baba yake mkubwa, kwa kuwa akiripoti katika gereji yake kila asubuhi na kushinda hapo huku akimfuatilia kila analofanya katika magari, Mzee Hamis, baada ya kuona kuwa Nusra alikuwa na moyo wa kweli wa kujifunza ufundi, aliamua kuanza kumfundisha ufundi hatua kwa hatua.

Baada ya kumudu kidogo kishika Spana, Mzee Hamis, mwaka 1998, alianza kumfundisha udereva, tena kwa kumfundishia katika gari aina ya Comb Volkswagen, ambapo baada ya miezi sita tu Nusra tayari alishamudu kuendesha gari na kutulia barabani.

Nusra alipomudu kufanya vurugu za barabarani, alikabidhiwa na baba yake mzazi, Canter ya Tani 3 na robo ili aweze kufanyia kazi ya kubebea mizigo, huku akikodishwa ambapo alifanya kazi hiyo kwa muda wa miaka miwili.

Hatimaye mwaka 2001, Nusra, aliamua kuachana na kazi ya kuendesha Canter ya kubeba mizigo na kuamua kuanza kazi ya kulima kwa Treka, ambapo alikuwa akikodishwa na wakulima na alimudu kulima hadi Heka 10 kwa siku kwa ujira wa Sh. 10, 000 kwa kila heka moja.

Mwaka 2003, Nusra alianza kuendesha Min Bus, huku akiwa na Leseni ya Class C baada ya wakati huo kudanganya umri ili aweze kupata uhalali ya kufanya kazi anayoipenda ya udereva.

Dereva Mwanamke wa Basi la la Shabiby, Nusra Maguluko, akizungumza wakati alipoalikwa mbele ya viongozi kutoa ushuhuda kuhusiana na kazi yake ya Udereva wa magari makubwa kama Mwanamke, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Jengo la Kampuni ya usafirishaji ya DHL, iliyofanyika siku za hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Nusra alialikwa katika hafla hiyo baada ya kuwa ni mmoja kati ya wanawake waliopata tuzo za Usafirishaji kutoka kampuni hiyo ya DHL.

Alifanya kazi hiyo ya kutoa huduma usafiri kwa abiria kutoka Wilaya ya Kiteto kwenda Vijijini hadi mwaka 2006, alipokabidhiwa Basi aina ya Fuso lenye uwezo wa kubeba abiria 40, nakutoa huduma hiyo ya usafirishaji wa abiria kutoka Wilaya ya Kiteto hadi Dodoma, kazi aliyoifanya hadi mwaka 2011.

Baada ya kuchoshwa na njia za Vijijini na kile alichodai kuaua kutafuta maslahi zaidi, Nusra, aliamua kumvaa, Mbunge wa Gairo, Mhe. Shabiby, na kumuomba kazi jambo ambalo lilimshangaza na kumuhoji kama anaweza kweli kuendesha gari kubwa tena la abiria.

”Baada ya kuniuliza swali hilo, mimi nilimjibu Mheshimiwa samahani wewe nisaidie unipe kazi, halafu ndiyo utaniona nikiwa kazini kama naweza ama siwezi, kwani najiamini na ndiyo maana nimekuja kwako”. alisimulia Nusra

Baada ya maongezi marefu ya maswali na majibu juu ya ujasiri wa Binti huyo, aliyeonekana mdogo akiwa na maelezo ya mambo makubwa, Mhe. Shabiby, aliamua kumwajiri, Nusra ambapo hadi sasa anapiga mzigo katika kampuni hiyo ya Shabiby, akiburuza Basi linalofanya safari zake Dar-Dom.

?Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkurugenzi wa DHL na Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Zanzibar, Rashid Seif Suleiman, wakiwa katika picha ya pamoja na Nusra Maguluko, wakati wa hafla ya uzinduzi wa jengo la DHL, hivi karibuni.

Hivi Sasa Binti huyo, anandoto za kufungua Chuo cha Mafunzo ya Udereva kwa wanawake, akiwa na lengo la kuwafikisha mbali wanawake wenzake ili waweze kuwa na ujasiri wa kuendesha magari makubwa na si gari ndogo pekee.

Kwa hatua hiyo sasa Nusra, ameanza kusaka wafadhili, ili aweze kutimiza ndoto zake hizo, ambapo amewaomba wadau mbalimbali pamoja na Serikali kujitokeza kumsapoti, ili kufanikisha kufungua chuo hicho chenye lengo la kuwainua Kinamama.


Kipindi cha ‘Ongea na Janet’ chapaa na kuitangaza Tanzania katika nchi nane za Afrika.

$
0
0

 Mmiliki na Mweneshaji wa kipindi cha ‘Ongea na Janet’ Bi. Janet Sosthenes Mwenda.

Sasa ‘Ongea na Janet’ inaonyeshwa katika Dstv kufuatia kuingia nao mkataba.

MO BLOG: Tulishuhudia uzinduzi wa ‘Ongea na Janet’ tukaanza kuona vipindi vikienda hewani hebu tuweke wazi yapi mafanikio uliyopata mpaka sasa..?

JANET: Mafanikio nilianza kuyaona kwenye vipindi 13 tu vya mwanzo ambavyo vilitengeneza ‘Season One’. Nashukuru Mungu ‘Ongea na Janet’ ilijulikana haraka sana, ikapata watazamaji wengi, ‘comments’ nazo zikawa nyingi, ‘changes’ zikawa nyingi nikajikuta kila ninapokwenda siitwi tena Janet naitwa ‘Ongea na Janet’.

Hilo lilikuwa ni fanikio la kwanza kwamba niliondoka kwenye media muda mrefu na niliporudi nikapokewa vizuri kwa hiyo nawashukuru kwanza watanzania wenzangu kwa hilo, nawashukuru sana mashabiki wa Janet kwa kunipa ‘love’ ukweli.

Lakini pia fanikio lingine lilikuja kujitokeza ambalo sikulitegemea kwa kipindi kile lilikuja kama ‘surprise’ kwangu kwani nikiwa sina hili wala line nikapata simu kutoka MNet-Dstv Nairobi wakaniambia kwamba shoo yangu wameipenda na wataichukua, wakati huo nikuwa nimesha ‘apply’ siku nyingi sana mpaka nimesahau.

Wakanipa na ‘amount’ nikakubali wakaniuliza unazo ngapi? Wakati huo ndio nimemaliza ‘Season One’ nikawaambia ziko 13 wakasema wangependa kama zingekuwa 26 nikasema sawa nitakaporudi ‘Season Two’ nitawapatia wakakubali.

Hivyo niliporudi ‘Season Two’ nikawa nimeingia kibiashara zaidi na Dstv wakawa wameni-‘support’ nikaweza kubadilisha set up nzima ya ‘Ongea na Janet’  na wakanipa hamasa zaidi na nikapata nafasi ya kuitangaza nchi yangu kwa na kwa sababu naoneka katika nchi nane (8) tofauti.

Pia nikagundua moja kwa moja kuwa sasa nimeingia kwenye ‘competition’ na watu nane wanaoziwakilisha nchi zao kwa maana ya kwamba Tanzania iko kwenye ‘competition’ ya ‘talk show’ na nchi nane za Afrika.

Mashabiki wangu nataka niwaambie kwamba nitajitahidi kuboresha kazi zangu na natamani Talk Show bora East and Central Africa itoke Tanzania.  

Mmiliki  na  Mwendeshaji wa Kipindi cha Ongea na Janet Bi. Janet Sosthenes Mwenda katika moja ya vipindi walivyofanya na  Bondia maarufu nchini Tanzania Japhet Kaseba.

MO BLOG: Ni nchi zipi ambazo ‘Ongea na Janet’ inaonekana Afrika..?

JANET: ‘Ongea na Janet ‘ inaonekana hapa nyumbani Tanzania, Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi, Sudan Kusini, Malawi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC), hivyo naweza kusema ‘Ongea na Janet’ bado ina kazi kubwa ya kufanya si kwa ajili yangu bali kwa ajili ya watanzania wote.

MO BLOG: Baada ya kuingia mkataba na Dstv nini kilifuata..?

JANET: Baada ya kuingia mkataba nao fanikio la kwanza ilikuwa ni kubadilisha ‘set up’ ya kipindi kama nilivyosema na fanikio lingine ambalo lilikuwa ni ndoto yangu ya siku nyingi ni kuanzisha kampuni yangu mwenyewe ambayo itafanya vitu ambavyo natamani kuvifanya na tayari nimeshaifungua.

‘Soon’ itaanza ku-produce yenyewe kipindi cha ‘Ongea na Janet’, lakini sasa hivi tuko kwenye production ya kipindi kingine ambacho ni product ya ‘Ongea na Janet’ kwa hiyo watanzania wakae katika mkao wa kula kwani nitawaletea vipindi vingine viwili japo sita tangaza mimi.

Kwa sasa hivi kampuni yangu inafanya ‘production’ kwa hiyo nimekuwa na Media House, kwa mfano ukija na movie yako tunakurekodia, ukiwa na series zako tunakurekodia, dokumentari yako tunakutengenezea.

Kitu kingine namshukuru Mungu Dstv wamezidi kunifungulia milango kwani wamenifanya kuwa ‘agent’ wao kwa hapa nyumbani Tanzania. Kwa hiyo nimekuwa katikati ya mpishi na mlaji upande wa filamu, series na vipindi kwa hiyo kama kuna mtu sasa hivi ana kipindi anataka kiende Dstv anakileta kwangu, sisi tunakihariri upya, tunakifanyia ‘sub title’ kisha tunakipeleka Dstv.

Ilimradi hiyo kazi iwe ni ya kwake mwenyewe na ameisajili COSOTA.

Janet Sosthenes Mwenda akiwa katika mahojiano na mgeni.

MO BLOG: Uwakala wa kusambaza movies hapa nchini ulikuwa na ukifanywa na watu waliokutangulia vipi kuhusu ushindani..?

JANET: Ushindani ni mkubwa haswa kwa mtu wa kati, kwangu mimi changamoto kubwa ni kwamba bado ni mpya, halafu watu hawajazoea kufanya kazi na mimi kwa hivyo hawajui. Isipokuwa sisi kiukweli kampuni tumejipanga vizuri kiutawala, kwa sababu kampuni ina wajumbe wa bodi, ina General Manager, ina Admnistrator kwa kifupi wafanyakazi sasa hivi wako 10.

Kingine tunacho kifanya katika kampuni yetu ni kwenda na muda, ukileta kazi yako then unakotaka iende waki confirm sisi tunapeleka ile zungusha zungusha sisi hapana. Na kama kazi yako iko chini ya kiwango tumakwambia ukweli kwa sababu watu wanafeli kwenye ubora wa picha na sauti.

Janet Sosthenes Mwenda akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa kipindi chake.

MO BLOG: Kama Janet Sosteneth Mwenda Ongea na Janet imekubadilisha lolote..?

JANET: Kwa kweli ‘Ongea na Janet’ imenipa ‘peace of mind’ kwa sababu ni kitu nilichokuwa natamani kukifanya  miaka mingi sana lakini sikuwa nikipata upenyo na kwa kweli naomba nichukue nafasi hii kuwashukuru ‘CLOUDS’ kwa sababu wamenipa ‘room’ nzuri sana yaani pale ni nyumbani kwangu, kwa maana ya kwamba ninapowahitaji wao tayari wapo kwa ajili yangu.

Na kuanzia hapo ndio changamoto zikaanza kuonekana, na nadhani kwa wakati ule nilikuwa mtu wa kwanza kutoka nje na kipindi, lakini sasa hivi vinaingia vingi na vitakuja vingi kwa kuwa tunaingia katika ‘Digitali’. Naushukuru sana uongozi wa CLOUDS kwa kunisaidia na wafanyakazi kwa kunipa ushirikiano.

Lakini tena sana niwashukuru wananchi wanaongalia ‘Ongea na Janet’ kupitia kipindi hiki nimegundua kuwa watu wengi walikuwa na mambo mengi ya kuzungumza ila hawakuwana pa kuzungumzia.

MO BLOG: Kipindi cha ‘Ongea na Janet’ kinarushwa hewani saa ngapi na katika televisheni zipi..?

JANET:  Kwa mara ya kwanza kilikuwa kikirushwa hewani saa tatu kamili kila Alhamisi na Clouds TV na kurudiwa siku ya Ijumaa saa nane mchana na Jumapili saa kumi na moja jioni.

Lakini niliporudi ‘Season Two’ ambayo ni kibiashara zaidi, nikaongeza sasa inaonekana Jumanne Saa Tatu na Nusu Usiku hadi Saa Nne na Robo na Alhamisi Saa Tatu usiku na marudio yapo.

 

MO BLOG: Vipi katika ratiba ya kipindi hicho kurushwa Dstv..? 

 JANET: Dstv ni Chaneli  158 SWAHILI AFRICA MAGIC wanaonyesha pia Jumanne na Alhamisi kama ilivyo hapa Dar es  Salaam na muda ni ule ule, ujanua nina mkataba mrefu kidogo na Dstv na pia sitegemei kuondoka CLOUDS.

MO BLOG: Unalipi la kuwaambia watanzania lolote lile sio la fani yako.

JANET: Kinachoniumiza naona kama amani inataka kupotea nchini mwangu hivyo mimi naomba tu wanaohusika watusaidie, kwa sababu ukitaka kujua ubaya wa kutokuwa na amani, anzia nyumbani kwako usipokuwa na amani na mtu unayeishi naye nyumba haikali au siyo.? Hivi sisi kweli leo tukawe wageni kwa watu? Hii kitu kidogo inaniumiza.

MO BLOG: Nikurejeshe hapohapo kama “Ongea na Janet’ kwa nini ukafikia kuongea maneno hayo..?

JANET:  Kwa sababu ukifuatilia sana kipindi changu vitu vingi ambavyo naongea ni kujaribu kutoa elimu kutokana na ama matatizo tunayokutana nayo, kujifunza kutokana na vitu ambavyo vinatukwaza kwenye maisha na kuwekana sawa.

Hata siku moja huwezi kuona nazungumzia uchochezi wa kitu Fulani, kipindi changu ni cha amani na namuomba Mwenyezi Mungu anisaidie angalau niwe mmoja wa waleta amani nchini kwa kinywa changu, kwa sababu kuna wengine wanaleta amani kwa peni si ndio? Lakini mimi kwa kinywa changu niweze kuleta amani.

Kwa hiyo namuomba mtu yeyote ajifikirie kabla hajafanya chochote, hata kama umekasirika kiasi gani, jiulize nikishafanya hivi faida yake nini? Hata huyo unayemuumiza, ukimuumiza unafaidika nini. Kwa hivyo kila mtu ampende na amheshimu mwingine kwa imani yake.

Wakati naiombea nchi yangu amani, naomba watanzania wajue kwamba vijana tumeamua kufanya kazi watupe support: naomba pia nichukue nafasi hii kwa vijana wenzangu ambao hawapendi kazi, hakuna njia ya mkato kwenye maisha.

Rais wangu alisema ‘MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA’ na mimi naongeza la kwangu ‘BILA KUFANYA KAZI HAKUNA MAISHA BORA’.

MO BLOG: Janet Sosthenes Mwenda Mo Blog tunakushukuru kwa kuzungumza nasi machache kuhusiana na maendeleo ya kipindi chako na pia kukupongeza kwa kuweza kufikia hapo ulipofikia na kukutaka usikate tamaa pambana utafika.

JANET: Akhsante sana ndugu zangu wa Mo Blog nanyi nawashukuru sana kwa kunithamini na kutaka kujua nimefikia wapi kwa faida ya watanzania. Na nawaambia watanzania hasa vijana wawe wanatembelea mtandao wa www.dewjiblog.com watapata habari nyingi za kuelimisha, kufurahisha, burudani , michezo na pia kuangalia nafasi za kazi zinapotolewa.

MO BLOG:  Waambie watambue !! Ciao..!!

JANET: Ok Bye.!

 

Sunshine vitamin ‘may treat asthma’.

$
0
0

sunshine_8-t2

 

The amount of time asthma patients spend soaking up the sun may have an impact on the illness, researchers have suggested.

A team at King’s College London said low levels of vitamin D, which is made by the body in sunlight, was linked to a worsening of symptoms.

Its latest research shows the vitamin calms an over-active part of the immune system in asthma.

However, treating patients with vitamin D has not yet been tested.

People with asthma can find it hard to breathe when their airways become inflamed, swollen and narrowed.

Most people are treated with steroids, but the drugs do not work for all.

Video ya Mahojiano na Balozi wa Umoja wa Afrika (AU) Mhe Amina Salum Ali.

$
0
0

Karibu katika sehemu ya kwanza naya katika mahojiano kati ya Jamii Production na Balozi wa Umoja wa Afrika (AU) nchini Marekani Mhe. Amina Salum Ali.

Sehemu ya kwanza:-

969198_478791605539945_1876227749_n

 Mwanachanga moto yetu Mubelwa Bandio ana kwa ana na Balozi wa Umoja wa Afrika (AU) nchini Marekani Mhe. Amina Salum Ali. 

Katika sehemu hii, Mhe Amina ameeleza mengi ikiwemo…

1: Historia ya maisha yake.

2: Aliingia vipi kwenye kazi ya diplomasia?

3: Ni nini wajibu wake? Anawajibika kwa nchi ya Marekani ama na mashirika ya kimataifa kama IMF na World Bank?

4: Ni wapi ulipo mpaka kati ya majukumu ya mabalozi wa nchi wanachama wa AU na yeye anayewakilisha Umoja?

5: AU ina mikakati gani katika kufunda ama kuwalea viongozi wa afrika?

6: Kuna MAFANIKIO GANI ya Umoja wa Afrika hasa ukizingatia kuwa tangua kuanzishwa kwake tumeshuhudia nchi zikizidi kugawanyika badala ya kuungana kama Ethiopia na Eritrea na hata Sudan na Sudan ya Kusini?

7: Ni nini kinachokwamisha Umoja wa Afrika katika migogoro kama ya Kongo?

8: Nchi zetu ziko huru, zinajitawala, lakini ni kwa MANUFAA YA NANI?

9: Ni kweli kuwa Umoja wa Afrika unaendelea kuwepo si kwa mafanikio yake, bali kwa kukosekana kwa UMOJA M’BADALA?

10: Ni kweli kuwa kuna mamluki wanaokwamisha harakati za Umoja wa Afrika toka nje ya bara letu?

11: Tofauti ya mifumo ya utawala na nguvu za kijeshi na uchumi zinaathiri vipi UMOJA WA AFRIKA?

KARIBU UUNGANE NASI

Africa leaders not good enough for award – Mo Ibrahim

$
0
0

Mo Ibra- photo

Billionaire Mo Ibrahim discusses why no African leader qualifies for the $5m governance prize he sponsors.

Sudan-born telecoms tycoon Dr Mo Ibrahim says rising inequality is destroying social cohesion

The Mo Ibrahim Prize for Achievement in African Leadership is the world’s most generous prizes. It is also proving to be one of its most elusive, after the prize committee announced on Monday that there was no African leader who met the criteria for the 2013 award.

This is the second year in a row that no suitable candidate has been found. Since its inception in 2007, the prize has only been awarded three times.

Dr Mo Ibrahim, a Sudanese-British telecoms tycoon and philanthropist, established the London-based Mo Ibrahim Foundation to help inspire good governance and exceptional leaders. By finding so few candidates that meet its standards, critics of the award argue it reinforces negative stereotypes about African leaders.

Al Jazeera’s Yasmine Ryan spoke with Dr Ibrahim about why the foundation is finding it so hard to find awardees, the relationship between rising inequality and worsening rule of law, and the controversy surrounding the International Criminal Court’s (ICC) focus on African leaders.

moibrahim

Al Jazeera: Were there any leaders who might have qualified who were under consideration for the Mo Ibrahim Prize this year?

Mo Ibrahim: Yes of course, I’m not a member of the prize committee, but according to the rules, the committee looks at the people that left office in the last three years, peacefully. It is up to the prize committee to decide whether people meet the standard. We set a very high standard, of course. And we are proud of our prize committee for being credible and tough. It’s a prize for excellence, it’s not a pension.

The Mo Ibrahim Prize A $5-million award followed by $200,000 a year for life

Winners include Botswana’s Festus Mogae, Mozambique’s Joaquim Chissano.and Cape Verde’s Pedro Verona Pires

Eligible leaders must have been democratically elected and have left office peacefully within the last three years

AJ: Do you think it’s time to expand the prize, perhaps to include the many non-heads of state who are playing a positive transformative role?

MI: We created a brand, a prize, for a specific reason. We should not tinker with that. If there is a need to offer prizes to wonderful parliamentarians, to great newsmen or women, to footballers, or whoever, that’s fine. But we should not just mix up things together and destroy the brand we have just because one or two years we don’t have a winner.

 Africa-MoIbrahim-10132011

What is the objective of this? It’s focusing on presidents as tools to change their countries, given the power they have. We have not cornered the market on prizes and we invite everybody else to offer prizes for civil society, for the best NGO, for whatever.

Ourselves, we offered a different kind of prize for the Archbishop Desmond Tutu. This was a prize for a brave man who spoke truth to power.

AJ: The Nobel Peace Prize committee is, interestingly, often criticised for the opposite reason; for not being selective enough. Do you think the Nobel Peace Prize committee could learn something from the Mo Ibrahim Foundation?

MI: I will not start by criticising the Nobel Peace Prize committee, because on my committee we have three Nobel Prize winners, and I’m afraid to upset them! [Laughs] So I pass, no comment.

AJ: The Ibrahim Index of African Governance ranking countries according to their performance was also released today. You have said that the information collated in the index is an important empowering tool for citizens in the countries surveyed. In what ways can citizens use this information?

From the 2013 Ibrahim Index of African Governance

MI: This is a scorecard. It shows exactly what has been achieved over the last 13 years. We’ve been publishing very detailed data over 13 years. We have 133 parameters we measure. It gives people full details: How effective is the police force? How effective is the judiciary? Women’s social and economic rights…

This is a wealth of information, for people to see what is strong, to keep doing it, and what needs to be fixed. It also gives an opportunity to compare your performance with that of your neighbour, to enable conversations, peer review. We can pick up the phone and say “What are you doing here”?

Every time I meet an African president, they open up the index. They love it, because it can help them improve their performance.

mo-ibrahim

AJ: The index shows that the gap between the best and worst countries is widening. Do you think this growing inequality is a uniquely African issue, or you think it is part of a global trend?

MI: There are two areas of inequality. One issue is that we see that eight countries have been in the top ten since the beginning of our data collection. It seems the guys who got it right, they build their institutions and it keeps them on the right path.

At the bottom, actually there have been a lot of changes. The best improvement, actually, has been from some of the countries at the bottom, that managed to get out of poverty and did not fall back into the vicious cycle of poverty.

The second part [of the issue of inequality] is that the fruits of the economic progress, somehow appear to be limited to the top one percent of the population. That is producing a widening gap between the wealthy and the poor. That produces tension. This phenomenon is not just an African phenomenon, it’s happening in the US, it’s happening in the UK, it’s happening everywhere.

This is dangerous. You are building tension inside society. You will reach a point where social cohesion is destroyed.

AJ: The index also showed a trend of worsening levels of personal safety and the rule of law. What are the factors driving these trends?

MI: I just told you.

AJ: That it’s due to the inequality?

MI: Exactly. Most of the violence before was happening because of tensions and hostilities across borders. Now it is happening because of conflict within the country. We need to look [at] why are we are lacking social cohesion.

From the 2013 Ibrahim Index of African Governance.

AJ: You’ve spoken in the past about how Africa’s youthful population gives it the possibility of becoming the next “factory of the world”. Which countries do you think are best place to do this?

MI: I wouldn’t like to pick one country. I think the country that’s going to do this is the country that’s going to produce a better education for its young people, better training for young people. We need people who are able to serve the new economy. We need people who are versed in the new software, people who are good with their hands, smart kids.

AJ: Kenya’s President Uhuru Kenyatta has called the International Criminal Court “imperialist and racist”, and there are many African leaders who agree with him. Do you think there is any truth to their assertion that the ICC has targeted African leaders unfairly? If so, what’s the alternative?

MI: I think there’s a need for a serious conversation between the African Union and the ICC. On one hand, the allegation that the ICC has only tried or prosecuted African leaders is correct. Do atrocities only happen in Africa? What is happening in Myanmar, what is happening in Baghdad? Where is the ICC? That’s a valid question.

On the other hand, Africa has no alternative to the ICC. We don’t have an African criminal court that is capable of really trying crimes against humanity. So when we have victims in Africa – and we do have victims in many cases – who can give them justice?

Instead of throwing out the baby with the bathwater, we need to find a way to reconcile the two. We need to find a way to the ICC so that it doesn’t become just a political tool, as it is perceived by some African leaders

Global governance is in crisis. Do we say “let us withdraw from the United Nations”? We love the United Nations, we need the United Nations, what we need to do it to try and reform it, because we need it.

That is the same approach we need to take with the ICC and some of these other global governing bodies. Let’s be cool-headed, and find a way to move forward.

Source Aljazeera 

Dada mwenye Kipara, mrembo na wa Kawaida

$
0
0

nemela1

Na Muhidin Issa Michuzi

Mlimbwende na mwanamitindo Flaviana Matata aliufanya mtindo huu uwe maarufu pale aliposhinda taji la Miss Universe Tanzania mwaka 2007, na kuwakilisha nchi kwenye mashindano ya Miss Universe mwaka huo huo, ambako aliibuka mmoja kati ya washindani 15 bora katika nusu fainali na kushika nafasi ya sita katika fainali.

Flaviana  alikuwa mshiriki wa kwanza Mtanzania wa kwanza kushiriki kwenye mashindano ya Miss Universe, naye alishindana akiwa amenyoa upara kwa mshangao wa wote. Hivyo ghafla tu upara ukawa mtindo mkubwa kwa wakinadada nchini.

Ni kweli kwamba mlimbwende huyo aliupa umaarufu mkuwa mtindo huo wa wasichana kunyoa upara, ila sio uwongo kwamba kuna wasichana ambao wanauchanganya  na maisha ya kawaida kwa mafanikio makubwa japo unaonekana ni wa walimbwende tu.Mmoja wao ni Nemela Mangula, msichana makini aliyezaliwa na kukulia Tanzania katika familia ya watoto sita ya – naam, umepatia kabisa  – Mzee Philip Mangula, Makamu Mwenyekiti wa chama tawala cha CCM  (Bara).

“Kwa kweli baba na familia kwa ujumla wamekuwa wakinipa moyo  katika mtindo huu wa kunyoa upara; kila mara walikuwa wakiniambia kwamba nifanye kile roho inapenda na kuniacha na amani moyoni

“Huu ni mtindo ambao nilikuwa natamani kuujaribu kila mara: ila nakumbuka wakati Fulani ya majira ya joto nikiwa naanza mitihani yanhgu ya mwisho nilikuwa nachukua muda mrefu kujiandaa asubuhi kwa sababu ya nywele. Na huo ukawa ni muda muafaka wa mimi kujaribu mtindo wa kipara.

“Ilinichukua siku kadhaa kuuzoea lakini mara nilipokwisha uzoea ilikuwa ni kama mtu aliyekombolewa, maana kila kitu kikawa chepesi”, anaelezea, akiongezea kwamba la hasha, yeye hana matatizo ya macho bali miwani anayokuwa amevaa kila mara ni mambo ya urembo ama mtindo tu, na wala siyo ya macho.

 Mara ya mwisho wa yeye kuwa na nywele ndefu ilikuwa mnamo mwezi wa Mei mwaka 2010, wakati wa mitihani yake ya mwisho. Wakati huo alipendelea kuchana nywele zake, lakini kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya huko Wales alikokuwa anasoma, ikamlazimu awe anasuka ama atengeneza rasta kuzifanya nywele zake ziwe na afya.

Nemela, asiyependa makuu, haamini kwamba kila aendako macho yote humkodolea yeye, hasa hasa anapokuwa ameongozana na baba yake kwenye shughuli mbalimbali za kitaifa. Hali kadhalika huwa hajisikii vinginevyo awapo mbele ya kadamnasi, akisisitiza kuwa popote alipo na wakati wowote yeye yuko poa tu.

nemela2

 “Kama kumbukumbu zangu zitanitendea haki; baba aliponiona nikiwa nimenyoa kipara kwa mara ya kwanza alisema “Hii ni dalili njema kwa maana  kikawaida maprofesa wote na madaktari hupata kipara nusu kichwa tu, na wewe una kipara kichwa chote ikimaanisha unafanya vyema masomoni”,anakwambia Nemela mwenye umri wa miaka 25, huku akiachia bonge moja la tabasamu.

Anakataa katakata kwamba kunyoa kipara kunahitaji moyo na kitu kinachoweza kufanywa na  wanawake walio jasiri tu ambao wanakubali kokodolewa macho kila waendapo.

Nemela anashukuru moyo anaopewa na familia yake, na ni kweli kabisa kwamba ameshawahi kujaribu mitindo ya nywele ya kila aina na yote amekuwa akiipenda.

“Ila sema nilipoamua kunyoa kipara nikajiambia kwamba hii ndiyo yenyewe”, anakumbuka Nemela mwenye shahada ya Sheria kutoka chuo kikuu cha Glamorgan cha Cardiff,  Wales, pamoja na stashahada ya Uhusiano wa Kimataiafa na Diplomasia toka Chuo Cha Diplomasia cha Kurasini, Dar es salaam.

Hata hivyo anakiri kwamba ni wanawake wachache wa Kiafrika wanaopenda kunyoa kipara, akikazia kwamba yote hayo hutegemea ni namna gani mtu atajisikia kuwa na amani.

“Hakika siwezi kumshauri mtu anyoe kipara kama hawatokuwa na amani moyoni katika mtindo huo.

“Pengine ushauri wangu kwao ni; Kinamama na kinadada, chagueni aina ya mtindo wa nywele unaokupendeza, mtindo ambao utakufanya uwe na amani moyoni na kukupa muonekano wa kipekee”, anakueleza kwa unyenyekevu unaoficha kabisa alama zake za kuwa mtu mwenye rekodi nzuri ya usomi nyuma yake.

 Na hapo unazungumzia msululu wa tuzo alizokuwa anapata toka akiwa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya St. Francis, tuzo ya kutukuta toka kwa Waziri Mkuu wa Bunge la Taifa la Wales, kwa watu wanaojituma na kujitolea katika kutumikia jamii.

That is not all. The bald lady who is presently working at Kijani Agro Tanzania LTD., in Dar es salaam,  is also a former President of the student government at The Centre for Foreign Relations.

Does she believe that whatever men can do women can do better?

“Actually, I believe that the ability, skill or capacity of an individual does not at all depend on their gender. The brain is the most amazing feature on our bodies; scientists to date are still trying to understand it. They haven’t proved that one sex is somehow superior to the other when it comes to intelligence; they simply illustrate how the brains of men and women have different weaknesses and strengths.

“Thus my point being; women and men are both capable of achieving the same success, one doing better than the other depends on a number of reasons like a certain lifestyle, an upbringing, their surroundings but mostly the amount of effort/ determination they have.

“One among my favourite quotes by Robert Anthony is “You can have anything you want if you are willing to give up the belief that you can’t have it.”

“Therefore if one believes that they can achieve something, there is no reason they shouldn’t do it as good as anybody else or even better”, she philosophizes.

Nemela is not interested in diving into politics, insisting that currently  she would like to focus on building  her career “I look forward to pursuing master’s degree in diplomacy and economic development. Let me say that at this time I want to accomplish my educational goals, all the same I aspire to become a representative of my country in the international arena” she explains.

In 20  years from now, Nemela envisions a peaceful United Republic of Tanzania 20, a society that has a reduced income gap between the highest paid person in the government and the person having the lowest income.

“A country with more female representatives; moreover I support the Tanzania development Vision 2025 that will see a halved proportion of people living below the national poverty line, reversed spread of HIV/AIDS, halved proportion of underweight, under-five year olds and  halved proportion of people without access to safe drinking water”, she says almost in a trance.

Also she sees Tanzania Achieving universal primary education, gender equity and  equal access for boys and girls to primary and secondary schools, reduced maternal mortality ratio by three-quarters, as well as reversed loss of environmental resources.

nemela4 (2)

Who is Nemela’s  number one Role model?  Mzee Philip Mangula, of course!

“First and foremost he has always been there for me, supporting my every dream. He has never let anyone in my family down; in fact he does more than enough!

“Not only is he a wonderful parent, his honesty, strength and philosophies are inspirational to many including me. He is my mentor, he defends the weak and stands for what is right! If there is one thing he has always set an example of, is being true to oneself and always depend on God because he is the only constant factor in our lives”, says Nemela, with the child in her almost jumping at you.

Her other role models include Rosa Parkes, who she says peacefully refused to move to the back of a bus – sparking waves of non-violent protest in favour of African-American’s rights, African-Americans went on to achieve full and equal rights in the USA. Had segregation and discrimination outlawed and took her stand to fight for her rights and made a difference!

The other role model for Nemela is Emmeline Pankhurst, leader of the suffragette movement which gained right to vote for women for the first time in 1919 Britain. “Because of her women are now allowed to vote in every democratic country in the world” she smiles.

nemela3

Who would you love to meet in life and why?

“I would like to meet Aung San Suu Kyi, the Burmese pro-democracy leader who has inspired the world with her non-violent resistance to a brutal dictatorship.

“Another person is Benny Hinn, he is my spiritual mentor, I listen to “this is your day” almost daily”, says Nemela.

She  would have also loved to meet Mwalimu Nyerere, adding that  few minutes with him would have definitely been life changing for her!

Nemela describes the Father of the Nation as  a charismatic and visionary leader and that she is a  big fan of all his philosophies and leadership style. Among her favourite Mwalimu quotes is “There must be equality because only on this basis will men work cooperatively. There must be freedom because every individual is not served by the society unless it is his. And there must be unity, because only when the society is united can its members live and work in peace, security and well-being. Society must have institutions which safeguard and promote both unity and freedom and it must be permeated by an attitude—a society ethic—which ensures that these institutions remain true to their purpose, and are adapted as need arises.”

You must have had harbored a need to talk something to the media when and if the chance arises, like today. Well, here you are today, Shoot…

Says Nemela. “In reality I never dreamed of having such an opportunity but now that I have, I would like to start off by saying thank you for such a wonderful opportunity. I am not a person of many words, however; I have a few inspirational quotes which inspire me and I would like to share them:

“Do not let what you cannot do; interfere with what you can do.”

–John Wooden

“Try not to become a man/woman of success but rather try to become a man/woman of value.”

–Albert Einstei

“It’s not about time, it’s about choices. How are you spending your choices?”

–Beverly Adamo

Last question: What is the meaning of your name, NEMELA?

“Ah hahahahaa…” I am a Mbena from Njombe. Nemela means “To be Proud of” or “love “, like

Unemela u Jesu is like saying I am proud of/love being inside Jesus…!

REST IN PEACE NEMELA.

Haijawahi kutokea nchini kwa mara ya kwanza Skylight Band inakuletea THE ROCK CITY CRUISE PARTY mkesha wa Mwaka mpya

Exclusive Interview: Brazil to host World Cup again after 64 years

$
0
0

Brazil is calling! Don’t miss the World Cup and Copacabana beach !

On Wednesday last week, MOblog hosted an exclusive Q and A interview with the Brazilian Ambassador to Tanzania, Hon. Francisco Luz, ahead of the upcoming World Cup Tournament. Read On; 

DSC_0076

MOblog Tanzania’s Chief Editor, Damas Makangale in an exclusive interview with the Brazilian Ambassador to Tanzania, Hon  Francisco Carlos Soares Luz at his office.

By Damas Makangale, MOblog Tanzania

MOblog: What was your initial reaction when you heard that Brazil will host the 2014 World Cup?

Ambassador Luz: I think like every Brazilian who is crazy about football, I was very excited with the news. At a time we knew that there was no competition since Columbia had retired its candidate so Brazil was standing alone. We knew [the World Cup] was supposed to happen in South America, so we are very happy and excited with the opportunity of hosting the world cup again after 64 years.

MOblog: Brazilians are going to the world cup with a squad of younger and very promising players compared to Spain, Germany and Argentina. To what extent do you think it will help the team to win the trophy?

Ambassador Luz: I think Scolari has done the right thing. He has mixed the team with young, talented players who are ready to present themselves to the world and become national heroes like Neymar da Silva Santos but he has included veterans; mature and experienced players.

MOblog: Do you think Brazil will benefit from a home advantage and go on to win their first World Cup since 2002?

Ambassador Luz: We have won the confederation cups and a home advantage will be a factor during the world cup finals. We believe that the home ground will make a difference to us.

MOblog: On a general note, do you prefer having 24 or 32 teams in the World Cup?

Ambassador Luz: I prefer having 32 teams because you have a real sense and taste of the World Cup because it involves all regions of the world.

MOblog: How confident are the Brazilian people and the media that Brazil will win?

Ambassador Luz: I believe the people are very confident after winning the confederation cup although it is not that easy. Some people are saying that winning the Confederation cup doesn’t guarantee that we will win the World Cup but the media is confident and they are ready to give accurate and balanced reports.

MOblog: Which cities in Brazil are the World cup matches being played in?

Ambassador Luz: The cities are Rio de Janeiro; where the final will be played at Maracana, Sao Paulo; where the first match will be held, Belo Horizonte, Salvador; Salvador where Africa meets Brazil. It a nice city and the food and music is really influenced by Africa. Other cities are Recife, Natal, Fortaleza, Manaus, Brasilia, Cuiaba, Curitiba and Porto Alegre.

MOblog: What do you think it will cost the average spectator to get to the World Cup and stay in Brazil?

Ambassador Luz: That depends on the fans. If you want see the initial matches, the cost is manageable but if you are planning to stay for the whole tournament, I think you need around 250 dollars a day including accommodation.

DSC_0028

MOblog: As of this moment are there still hotels available if one wanted to go for the World Cup?

Ambassador Luz: FIFA selected some hotels for their families and delegates but there are still other hotels available but prices are very high especially in Rio. The government is trying to talk to the Association of Hoteliers to avoid over charges. 

MOblog: What will the weather be like in Brazil during the World cup?

Ambassador Luz: During the world cup it will be winter to some parts of the country but the general weather will be nice and warm.

MOblog: Are there direct flights from Tanzania or Africa to Brazil?

Ambassador Luz: No, the best option is to go to South Africa; it is three hours to Johannesburg and nine hours to Brazil which is the shortest way.

MOblog: What are Brazil’s highlights and best tourist attractions for one to see whilst there?

Ambassador Luz: There are many wonderful tourist attractions in Brazil such as theaters, parks, Teatro Amazonas and the beautiful Salvador beaches but for Africans, I think they will enjoy Salvador the most. The music, the beaches and the food means they can feel at home. It is a really nice place and they sell African influenced food and like Bahia, Prawns and Beans which is delicious.

MOblog: The World Cup has sparked violence in the past. Have you taken any security measures in preparation?

Ambassador Luz: I don’t anticipate any violence or security problems because the government is fully prepared to tackle any violence or riots that may erupt during matches. This week all the security stakeholders, including the army, are going to have the meeting to finalise the security plans ahead of the tournament.

MOblog: Brazil has invested 9 billion dollars of taxpayer’s money into the World Cup, so what are the long term benefits that the hosting nation will get?

Ambassador Luz: Of course there are some infrastructure investments that will be accessible to the population long after the world cup. Stadiums such as Arena De Sao Paulo, Estadio Do Maracana, Rio de Janeiro, Estadio Do Maracana, Rio de Janeiro and Estadio Beira Rio, Porto Alegre all belong to private clubs which our National Development Bank (NDB) is financing for the tournament. Other investments have been made in the railway system, sub way system and we are upgrading the airports because we will have 200 new flights connecting the cities with Argentina, Uruguay and Colombia.   

DSC_0070

MOblog: What are the main economic impacts Brazilians are most likely to see after the World Cup tournament?

Ambassador Luz: The number of tourists arriving in Brazil will have an impact to the economy. There will be a lot of entertainment available during the matches. People will travel from one point to another and make the most of seeing Brazil. Tourist attractions will attract many people and bring good business such as Teatro Amazonas (Amazon theatre), rivers Negro and Solimoes and Natal City which is one of the most beautiful coastlines in the world.

MOblog: What do you think are the main areas of co-operation between Brazil and Tanzania which the two nations should focus on?

Ambassador Luz: We try to concentrate in agriculture and energy. Actually today I am receiving a group of researchers from the Agriculture Organization which co-ordinates the Brazilian agriculture policies and programs around the world. I am receiving the head of the organization from Africa to evaluate the five programs of agriculture in Tanzania. We also have project focusing on the health sector especially HIV/Aids. In the energy sector we have the Brazilian company PetroBras who are training Tanzanians in gas, oil and energy.    

DSC_0094

Some of the MOblog team in a group photo with the Brazilian ambassador to Tanzania.

DSC_0099


Uzinduzi wa Albamu ya Extra Bongo: Red Carpet ya Dar Live!

$
0
0

Baadhi ya safu ya wanenguaji mahiri wa kiume wa Extra Bongo.

Amini akishoo Love na Linah (kushsoto) pamoja na mwimbaji wake.

Baadhi ya safu ya wanenguaji wa kike mahiri wa Extra Bongo.

Wanenguaji katika pozi poa.

Khadija Kopa na Abdul Misambano wa TOT.

Khadija Kopa, Misambano na ‘Okwi’ shabiki wa Yanga.

Lina na ‘back-up singer’ wake.

Mamaa Winnie Masanja, mama watoto wa mwanamuziki Banza Stone.

Mke wa ‘Mkubwa’ Said Fela (kulia).

Mmoja wa wanamuziki wa Mashujaa Band, Gado.

TX Moshi Jnr wa Msondo Music Band.

Wadau wa Dar Live.

Wasanii Linah na Amini.(Picha: Abdallah Mrisho/GPL)

Kutana na Doreen Peter Noni Mjasiriamali na mbunifu wa mavazi nchini

$
0
0

MOblog Tanzania hivi karibuni ilifanya mahojiano na Mjasiriamali na mbunifu wa mavazi nchini Doreen Noni aliyehudhuria mkutano wa Uchumi Duniani uliofanyika huko Davos, Uswisi (World Economic Forum) mwezi uliopita juu ya yote anazungumzia nafasi ya Wanawake, Vijana na Ujasiriamali endelea…….

DSC_0020

MOblog: Tafadhali hebu jitambulishe wewe ni nani?

Doreen: kwa jina mimi naitwa Doreen Esthezia Peter Noni

MOblog : Umezaliwa wapi?

Doreen: Nimezaliwa Dar es Salaam, mwaka 1989 mwezi wa tatu, tarehe 10 na nina kaka zangu wawili , mimi ni mtoto wa tatu na mwisho kuzaliwa  na wa kike pekee na wazazi wangu pia ni Wajasiriamali.

MOblog: Ulisoma wapi?

Doreen: Nilisoma Upanga Nursery School na baada ya hapo nikahamia Nairobi kuanzia darasa la sita mpaka form Six nilikuwa Brook High School, Nairobi.

 MOblog: Je chuo ulisoma wapi?

Doreen: Chuo nilisomea Uingereza, Nottingham Trent University na nilisomea mambo ya Multi Media.

Doreen-Noni-at-Davos

MOblog: Ulipata nafasi ya kuhudhuria mkutano wa Uchumi duniani(World Economic Forum 2014) hebu tueleze ulipata vipi nafasi ya kuhudhuria?

Doreen:  Mimi nilipata nafasi ya kuhudhuria (World Economic Forum) kupitia asasi ya Global Shapers ambayo ni delegation ya vijana kupitia World Economic Forum na vijana kuanzia  miaka 20 mpaka 30 ambao kazi yao kuu ni kuangalia vijana ambao wanaleta  mabadiliko katika jamii na ushiriki wa vijana katika maeneo mbalimbali, ya ujasiriamali kwa hiyo nilituma maombi kwenye jukwaa la Uchumi Duniani na wao wakaona nafaa kuhudhuria na nikahudhuria kwa hiyo nikawa mjumbe wa World Economic Forum kama kijana na jukwaa la kuwakilisha vijana wa bara la Afrika na nimehudhuria mikutano mitatu ya uchumi duniani mpaka sasa.

Doreen-Noni-Conference

MOblog: Je kwenye mkutano huu wa hivi karibuni nini kilijitokeza?

Doreen:  Nilikuwa kwenye session tofauti nilikuwa kwenye panelist mbalimbali, kama vile Innovation and Design na panelist nyingine ilikuwa Africa the next billionaire ambayo kulikuwa na marais mbalimbali kama vile Goodluck Ebele Jonathan; Rais wa Nigeria, Aliko Dangote; Afisa Mtendaji Mkuu wa Dangote Group na John Mahama; Rais wa Ghana, hii session ilikuwa inaogelea kuhusu umati wa watu Afrika na vijana tulikuwa kama 50 ambao tulihudhuria mkutano huu na vijana wengi Afrika wanatuma maombi duniani na kila session wanataka vijana wahudhurie kwa hiyo wanataka kujua uwezo wa vijana katika maswala mbalimbali ya kiuchumi, kijamii na kijamii.

MOblog: Je unafikiri nafasi ya Tanzania kwenye mkutano kama huu ikoje?

Doreen: Yaani kwa kweli ukiniuliza Tanzania kama nchi kwa kweli ni ngumu kwa sababu mimi sijakaa sana nchini na kwa sasa najifunza kuhusu nchi yetu lakini kwangu kwa kipindi kirefu sikuwepo hapa nyumbani. Lakini kwa vijana mikutano hii ni mizuri kwa kujifunza.

MOblog: Ulianza lini kazi yako ya ubunifu?

Doreen: Nilianza 2011 na kusajili kampuni yangu mwaka huo huo na inaitwa Miracle films and Studio, tuna shoot kazi mbalimbali films, matangazo na nilianza rasmi swala la ubunifu wa nguo mwezi wa Machi mwaka huo huo nikaanza taratibu na watu wakawa wananipa mrejeo (feedback) nzuri na (positive results) na ndiyo zimenifanya niendelee na kazi hii ya ubunifu wa mavazi.

DSC_0067

MOblog; Changamoto ngani umekutana nazo kwenye kazi yako hii ya film na ubunifu wa mavazi?

Doreen: Changamoto kama kijana self discipline, na kupata mawazo, cha pili ni Mental ship kama kuna watu wa kukupa mawazo ni vema na timu ya kufanya nayo kazi lakini mindset ya watu ni kupata pesa tu lakini mimi nataka kutengeneza Empire kwa hiyo ni muhimu kupata timu bora ya kufanya nayo kazi.

MOblog: Ni kitu ngani unapenda na nini hupendi?

Doreen: Sipendi uongo kabisa, wote ni watu wazima, mimi ninachopenda ni ukweli, kudanganya kunaleta matatizo mengi. Uaminifu ni muhimu inatuwezesha kuokoa muda kwa sababu ya ukweli, muda ni muhimu sana kwa maisha ya binadamu kwahiyo sipendi uongo kabisa, na kwa kupenda napenda wazazi wangu na marafiki zangu tu.

DSC_0129

MOblog: Umeolewa?

Doreen: Single!

MOblog: Nini siri ya mafanikio yako?

Doreen: Mindset (Mtazamo)

MOblog: Ukiwa mapumziko unafanya nini?

Doreen: napenda kusafiri kuongea na kukutana na watu tofauti lakini pia napenda kufanya mazoezi.

MOblog: Je watu wanaokuzunguka wanasemaje kuhusu wewe?

Doreen: Wana heshimu kazi yangu na kunitia moyo kwa kila kitu ninachofanya.

MOblog: Unazungumziaje hali ya wanawake hapa nchini na ushauri wako kwao?

Doreen: Wanawake wajasiriamali wawe wanafanya kazi kwa bidii lakini ni lazima wajitambue na malengo yao ya baadaye na kujipanga kwa ajili ya maisha yao. 

Skylight Band imebadili sura ya muziki wa laivu

$
0
0

DSC_0009

 Wamiliki wa Skylight Band Dk. Sebastian Ndege na Justine Ndege wakiwa kwenye moja ya show za vijana wao Skylight Band ndani ya kiota cha maraha Thai Village Masaki jijini Dar.

Na MOBlog Team

KAMA ni mpenzi wa muziki hutasita kukubaliana nami kwamba tangu Skylight Band iingie katika ulimwengu wa muziki wa laivu nchini hapa, kuna mambo mengi yamebadilika hasa namna ya kutoa burudani hiyo miongoni mwa bendi ambazo zilikuwapo au tuseme zipo hadi sasa.

Bendi hii ambayo ilianza 2011 imekuwa tishio kutokana na aina yake ya muziki wanayoipiga ya Afro Pop.

Hivi karibuni kutokana na mafanikio hayo yanayoonekana dhahiri hasa katika viwanja vya Thai Village na Escape One, Mo Blog ilipata nafasi ya kuzungumza na Mkurugenzi wa Skylight Band, Justine Ndege ambaye yeye na ndugu yake Dk Sebastian Ndege ndio wamiliki wa bendi hiyo.

Kwenye mazungumzo hayo na Zainul Mzige wa MOblog ilitaka kujua jinsi wazo la kuundwa kwa bendi hiyo lilivyofikiwa,uundaji wenyewe ulivyokuwa, mikakati ya kujitambulkisha na kujua hali ya baadaye ya bendi na changamoto zake.

DSC_0096

Wanamuziki wa Skylight Band wakitoa burudani kwa mashabiki wao kwenye uwanja wao wa  nyumbani kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar kila siku ya Ijumaa wanakuwa hapo kuanzia saa tatu usiku: Kutoka kushoto ni Joniko Flower, Mary Lucos, Sony Masamba, Aneth Kushaba AK47 na Sam Mapenzi wakiwajibika jukwaani.

MO BLOG : Naomba kabla ya kuanza kwa mazungumzo jitambulishe kwa wasomaji wetu.

SKYLIGHT: Mimi naitwa Justine Ndege ni mkurugenzi wa skylight band na Skylight entatainment. Skylight ni bendi ya ndugu wawili, Dk Sebastian Ndege na Justine Ndege na wote ni wakurugenzi; sisi ni kaka na mdogo.

MO BLOG :Unaweza kutuambia namna mlivyofikiria kuanzisha bendi hii?

SKYLIGHT: Wazo la kuanzishwa kwa Skylight Band lilifanyika wakati tukiwa katika burudani, mimi na ndugu yangu.Tukiwa tunakunywa na kuangalia mambo yanayoendelea pale.Katika mazungumzo tukasema kuna kitu kikubwa tunaweza kukifanya kuboresha mazingira kama haya badala ya kunywa na kuzungumza na marafiki pekee.

Katika mauzngumzo tukasema kwanini tusiwe na bendi ya kuburudisha.

DSC_0108

Sehemu ya wanamuziki wa Skylight Band wakitumbuiza mashabiki wao wakiongozwa na Meneja wa Bendi hiyo kutoka kulia ni Aneth Kushaba AK47, Digna Mbepera, Sony Masamba a.k.a Fally Ipupa wa bongo na Hashim Donode.

MO BLOG: Ilitokea tu wazo la kuwa na bendi au kuna kitu kiliwasukuma?

SKYLIGHT : Ni wazi kipo kitu kilichotusukuma ndio maana tukawaza. Tulitaka kubadili mambo katika burudani.Huko nyuma Dk Sebastian Ndege alikuwa anafanya mambo ya ushereheshaji yaani mc, alikuwa DJ na alikuwa na vifaa vya muziki.Tukasema basi hebu tujaribu .

MO BLOG: Mlipoamua kwamba tujaribu nini cha kwanza mlikifanya, mliitisha vyombo vya habari kama wengine wanavyofanya tunataka hiki?

SKYLIGHT: Ha ha ha unaenda kasi sana, hapana. kwanza lazima uwe na mtu ambaye unajua anaweza kutengeneza mambo fulani. Kwa hiyo mtu wa kwanza kabisa kumfikiria ambaye tulishawahi kufanyanaye kazi alikuwa ni Aneth Kushaba. Tukamwambia basi tukutane nyumbani kwa Dk Sebastian na akafanya hivyo. Ndio kusema Skylight iliundwa nyumbani kwa Dk . Sebastian Ndege mwaka 2011.

Pale Aneth alichukua jukumu la kukusanya.Tukasema hebu Aneth kusanya watu tuone kama inawezekana. Muziki wa kwanza muziki wa pili tukasema inawezekana. Tukasema twende kazini kuleta changamoto kwenye muziki wa laivu.

DSC_0116

MO BLOG :Naam mazoezi yamefanikiwa baada ya hapo burudani mliianzishia wapi?

SKYLIGHT: Tulifanya utafiti wa kutosha, tukajaribu kufuatilia ,tukachekecha kuona tutaanzia wapi, tukapata sehemu yetu ya kwanza ilikuwa Mafia Fishing Lounge. Tukaanza pale tukajaribu kuleta mashabiki, tukaweka strategy (mikakati) tofauti ya kujitangaza. Tukaweka matangazo katika maradio, kwenye mativii (televisheni) na kwenye Blogs. Kwa matangazo hayo, basi tunashukuru Mungu tulifika sehemu tukagundua kwamba watu wameanza kulewa muziki wa laivu na Skylight Band ni kitu gani.

MO BLOG: Inaonekana mambo yenu yanenda poa hamna shida yoyote ukiangalia jinsi watu wanavyowashabikia?

SKYLIGHT: Changamoto kiukweli zipo lakini mpaka leo tunamshukuru Mungu tumepata mashabiki kutoka sehemu mbalimbali.Kiukweli chalenge (changamoto) ni nyingi sana zikiwemo gharama za kuweka wasanii , kuwatunza, kuwapa mishahara kuwahudumia, lakini tunashukuru Mungu mambo yanaenda vizuri.

MO BLOG: Mambo gani hasa mmejifunza kama menejimenti toka muanze kutoa burudani 2011?

SKYLIGHT: Toka tumeanza kufanya burudani jambo zuri tumegundua kwamba mashabiki wanatoka sehemu mbalimbali kila mkoa, kila kata kila sehemu na uzuri ni kwamba unaweza kusikia jina kubwa la Skylight, lakini ukija kwenye shoo zetu ambazo tunazifanya kila Ijumaa na Jumapili za public (zisizobinafsi)  kiingilio ni reasonable (kinachowezekana kwa nafasi yetu kiuchumi). Unaposogea unakuta kiingilio sh elfu 5 Thai village; unaposogea Escape One unakuta kiingilio sh elfu 7, yote hayo yanatokana na strategy (mkakati) yetu ya kuleta au kuweka mabadiliko au changamoto kwenye muziki wa laivu.

DSC_0244

Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK47 akiwajibika jukwaani.

MO BLOG: Kwanini mfikirie kwamba mkakati wenu ndio hasa unaoleta changamoto?

SKYLIGHT: Kwa sababu mpaka tunaanza kufanya muziki wa laivu na kuweka Skylight Band, muziki wa laivu ulikuwa kama umeanza kupwaya kidogo kwa Sio tunafikiria tunaona. Kuna mabadiliko mengi katika muziki wa laivu tuliyoyasababisha. Bendi nyingi sasa, mathalani zinatumia mitandao ya kijamii kujitangaza. Sisi tulianza na mkakati wa kujitangaza kwa kutumia mitandao ya kijamii, tukisema jamani kuna kitu kipya mtaani kuna bendi inaitwa Skylight. Tukatumia picha, tukatumia maelezo, tunaionesha jamii, nayo ikatukubali. Ndio maana sasa hivi unaona kweli bendi sasa zinatumia mitandao ya kijamii. Tunashukuru sana wadau  wa mitandao ya jamii, tunashukuru MOBlog  na Zainul Mzige Meneja Mwendeshaji wake, wametusaidia sana, tuna mshukuru Haki Ngowi, LeMUTUZ, Jestina George, Global Publishers, Jamii Forum, Michuzi blog, DJ Sek Blog, DJ Choka, Wavuti, Vijimambo, Sunday Shomari, Fullshwangwe, Deo Rweyunga, Harakati za Bongo, Josephat Lukaza, Kajunason Blog, Kamera yangu, Bukoba Wadau, Gsengo, Michuzijr, Lukwangule Blog na wengine wengi kwa kuhakikisha kwamba Skylight inapata jina na kufika hapa ilipo. Lakini pia tunawashukuru mashabiki wameipokea vizuri bendi na wameiweka  Skylight juu.

MO BLOG: Wakati tunafikia mwisho wa mahojiano yetu unaweza kutudadavulia nini mipango yenu ya baadae?

SKYLIGHT: Plani zetu sisi ni kwenda zaidi, sasa hivi tunakwenda kimataifa tunatafuta masoko kimataifa kwa sababu tunaamini soko la nyumbani tumefanya tunachohitajika kufanya, japo yapo mengi tunayotakiwa kufanya.Kwa kuzingatia strategy yetu tunaamini kuna lengo tumelifikia kwa hiyo tunataka kwenda kimataifa.

MO BLOG: unaweza kutaja baadhi tu ya mafanikio hayo?

SKYLIGHT: Mengine tumeshasema kuhusu mashabiki kutukubali lakini ukienda katika medani ya muziki yenyewe mpaka sasa Skylight band imeshatengeneza nyimbo nane ambazo zinafiti albamu lakini zile ambazo zipo kwa umma sokoni ni nyimbo tano na video tano.

MO BLOG: Ningefurahi kama ungeliwatajia watu nyimbo hizo na zingine tatu zipo hatua gani?

SKYLIGHT: Nyimbo yetu ya kwanza inaitwa “WIVU ambayo ina audio na video , nyimbo yetu ya pili ni “NASAKA DOUGH” nayo ina video na audio nyimbo yetu ya tatu ni “CAROLINA” ina audio na video, nyimbo yetu ya nne ni “PASUA TWENDE” na nyimbo zote zinapatikana katika mtandao wa You Tube. Nyimbo yetu ya tano inaitwa “MAPENZI GANI” na ipo katika audio na sasa inatengenezewa video ambayo itakuja .

DSC_0231

Sehemu ya mashabiki wa Skylight Band wakicheza moja ya staili za bendi hiyo kwenye kiota cha maraha cha Thai Village Masaki jijini Dar ambapo kila Ijumaa bendi hiyo inatoa burudani kwa mashabiki wake.

MO BLOG: Pamoja na kwenda kimataifa nini kingine mmekifikiria huko mbeleni?

SKYLIGHT: Mipango yetu ya mbeleni ni kuhakikisha kwamba tunafanyakazi kwa kuangalia soko.Ila tunashukuru kwa Mungu ni kuwa mpaka sasa hivi strategy tulizozipanga zinaenda sawa tukimaliza ngwe ya kwanza tutaenda ngwe ya pili.

Projection (malengo) zetu ndani ya miaka mitano tunataka tuwe Afro Pop and Live Band, the best in Tanzania (bendi bora ya muziki wa laivu wa pop).Na hii inaonekana hata namna tunavyoingia kwenye tuzo mbalimbali. Kwa bahati nzuri au mbaya tumepata nomination (uteuzi) za mtu binafsi katika tournament za Kili Music  na tuzo zingine. Tunaamini mwaka mmoja ujao tutaingia katika kategori kama bend.

MO BLOG: Unaweza kmunitajia idadi ya wanamuziki na kazi wanayoifanya katika Skylight band?

SKYLIGHT:  Jumla wapo 16 na meneja wa bendi ni Aneth Kushaba. Safu ya waimbaji ni yeye Aneth Kushaba AK47, yupo Mary Lucos, Digna Mbepera, Joniko Flower, Sam Mapenzi, Sony Masamba a.k.a Fally Ipupa na Hashim Donode.

Kwenye vyombo wapo Idrisa  (mpiga drum), Baraka (mpiga drum), Emma ( mpiga bass), Danny Ki (mpiga bass), Tophy (mpiga bass) Amos ( mpiga kinanda),Daudi (mpiga tumba), Joshua Ngoje (mpiga solo) na Allen Kisso Mundele (mpiga solo).

MO BLOG: Una neno la mwisho?

SKYLIGHT: Ninalo.Tunawashukuru mashabiki wetu wote, wadau, waandishi wa habari tunaomba waendelee kutusapoti Skylight Band.

Andrew Nyerere; Mwalimu angekuwepo angepinga ufisadi!

$
0
0

Andrew Julius Nyerere

Kuna maswala kadha wa kadha yanayoikabili Tanzania kwa hivi sasa, miongoni mwa mambo haya ni sakata la akaunti ya Tegeta/Escrow, mchakato wa katiba mpya na mengine mengi. Mwandishi Nova Kambota amefanya mahojiano na Andrew Julius Nyerere ambaye ni mtoto wa kwanza wa baba wa taifa hayati Mwalimu Nyerere, fuatana naye katika mahojiano haya………………

SWALI; Kuna mambo kadhaa yaliyojitokeza siku za karibuni ambayo watu wanataka kufahamu manufaa yake kwa taifa, moja ya matukio hayo ni ziara ya Jafar Mermo  Idd Amin mtoto wa rais wa zamani wa Uganda marehemu Idd Amin mwaka 2008, je ziara hiyo ambayo ilimkutanisha na Madaraka Nyerere walipozuru Butiama ilikuwa na manufaa gani kwa taifa?

JIBU; Kwa familia ya Mwalimu Nyerere na familia ya marehemu Idd Amin nadhani ilikuwa jambo zuri kuleta upatanishi, kuhusu kama taifa lilipata faida sijui. Aliongea Jafari kuhusu kuanzisha mfuko wa hela kuwasaidia wanajeshi walioathirika na vita vya Kagera(wa Uganda na Tanzania), pia nchi hizi mbili zilihitaji kupatanishwa , Jenerali Musuguri alikuwa anaongea katika redio miezi michache iliyopita, kwamba wanajeshi wetu walikuwa na hasira sana, kabla ya kufika Kyaka walikuwa wameshawaua watu 10,000(elfu kumi), Jenerali Musuguri yupo hapa Butiama, natamani kwenda kumuuliza kama hao wote waliouwawa walikuwa ni maadui kwasababu hii ilikuwa ni vita yetu ya kwanza, inawezekana makosa yalifanyika.

SWALI; Una maoni gani kuhusiana na mwenendo wa CCM iliyoasisiwa na Mwalimu Nyerere ambayo sasa baadhi ya viongozi wake wanatuhumiwa vikali kujihusisha na ufisadi? Hudhani ni sababu tosha kwa watanzania kuikataa CCM ikiwa inakiuka misingi ya kuundwa kwake?

JIBU; CCM iliamua kujiita Chama Cha Mapinduzi kwa maana ya mapinduzi yaliyofanyika Urusi au Uchina, kwa maana kwamba watu walio wengi wakiwa na njaa wataleta fujo za kuiangusha serikali kama wamechochewa au hata kama hawajachochewa. Iwapo CCM itaendeleza hayo mapinduzi wananchi wataendelea kuichagua, inategemea tu watu wangapi bado wanaamini inaendeleza mapinduzi, maoni yangu mimi siyo muhimu, watu waamue, na nadhani wanaweza kugawanyika katika maamuzi.

SWALI; Miaka ya karibuni kumekuwa na watu wanaohoji namna baba wa taifa Julius Nyerere alivyoaga dunia, baadhi ya wanasiasa wametilia shaka mara kadhaa kifo chake mpaka ikampelekea Madaraka Nyerere kutoa kauli, vipi mtazamo wako kuhusu hili? Kuhoji kifo cha Nyerere kuna maslahi yoyote kwa taifa?

JIBU; Magige , mtoto wa Mwalimu anasema kuna chanjo moja ilikuwa wapewe watanzania ambayo Mwalimu alikuwa ana mashaka nayo. Mwalimu alimwambia Dr Mwakyusa kwamba yeye apewe, aijaribu halafu akiridhika ataiidhinisha wapewe Watanzania, lakini alipopewa hiyo chanjo, Mwalimu hali yake ilibadilika ghafla, amefariki. Niliposikia hiyo stori nilimweleza Magige kuhusu Global 2000 Report ya Warren Christopher, inasemekana katika miaka ya sabini viongozi wa Afrika walishauriwa na IMF wakubali wananchi wao wachanjwe chanjo za magonjwa ili watu wapungue ili iwe rahisi kuwasaidia; kwamba tatizo la kuwasaidia ni tatizo la logistics tu. Inasemekana ushauri huo ulikubaliwa na viongozi wetu. Global 2000 Report ni Top Secret ipo United Nations na hata ukiwa kule huwezi kuipata mpaka uwe na Special Clearence. No, nilimwambia Magige hatutapata faida yoyote tukianza kuuliza maswali kuhusu kifo cha Mwalimu, kama kuna mtu anabisha kwamba World Health Organization inaweza kufanya ufisadi, mtu huyo huwa anashauriwa kufanya utafiti jinsi W.H.O ilivyoanzishwa.

SWALI; Unazungumziaje mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya nchini, kutokana na matukio yanayoendelea kujitokeza kama Mzee Warioba kupigwa na hali ya kutoelewana miongoni mwa watanzania, Je unaona wapi tumekosea? Nini kifanyike kunusuru mchakato huu ili tupate katiba itakayolivusha taifa letu kutoka hapa tulipo?

JIBU;  Hakuna matatizo kuhusu katiba , isipokuwa kama kuna maoni yanayoweza kuiboresha katiba , maoni mapya ambayo siyo ya UKAWA , sasa ndiyo wakati wa kuyatoa.

SWALI; Unazungumziaje uongozi wa baba wa taifa hayati Mwalimu Nyerere? Una lipi la kusema kwa kumlinganisha na viongozi wa zama hizi?

JIBU; Sioni sababu ya kuwalinganisha viongozi wa awamu tofauti, zama tofauti zinahitaji viongozi, kumlinganisha Nyerere na Kikwete hiyo itakuwa sawa kumlinganisha Bismark na Angela Markel.

SWALI;  Unazungumziaje harakati za vyama vya upinzani nchini kupambana na ufisadi kama wa hivi karibuni wa Tegeta/Escrow? Unadhani vyama hivi vya upinzani vina dhamira ya dhati kupambana na madudu?Je vitafanikiwa?

JIBU;  Vyama vya upinzani vina nia njema , hii kashfa inayojadiliwa sasa hivi Bungeni imeletwa na upinzani. Hii vita ya sasa hivi ya Bungeni wanaweza kushinda, lakini kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa ni jambo lingine.

SWALI; Kadri ulivyomwelewa hayati Nyerere, unazungumziaje kutokuwepo kwake? Je unadhani angekuwepo angesaidia vipi kunusuru taifa kwenye kupambana na ufisadi na kunusuru mchakato wa katiba mpya?

JIBU; Mwalimu angekuwepo angepinga ufisadi, kuhusu katiba hakuna tatizo kubwa au naweza kusema hakuna tatizo lolote zaidi ya fujo inayoletwa na UKAWA.

 SWALI;  Ukipewa nafasi ya kuwashauri vijana wa sasa wa Tanzania, ungependa wafanye nini kulisaidia taifa lao?

JIBU; Vijana wa Tanzania wafikiri sana kabla ya kuwachagua viongozi.

SWALI; Unapata tafsiri gani unapoona taasisi za kidini kama kanisa katoliki likianzisha, kusimamia na kuratibu mchakato wa kumtangaza hayati Mwalimu Nyerere kuwa Mtakatifu?

JIBU; Kanisa katoliki ndiyo linataka Mwalimu aitwe lay saint, Mwalimu aliishi maisha ya uadilifu lakini kama alikuwa mtakatifu hiyo ni kwa Vatican kuamua.

SWALI; Unaweza kueleza nini kuhusu siku za mwisho za uhai wa Mwalimu na namna alivyokuwa akilalamikia ubinafsishaji/uuzwaji wa mashirika ya umma kama benki ya taifa ya biashara NBC, ukizingatia hali ya ugonjwa wake na uzalendo wake kwa nchi, alikuwa mtu wa namna gani? Alionekanaje nyakati zile?

JIBU; Uuzaji wa mashirika ya umma au ubinafsishaji siyo jambo baya wakati wote.

 Swali; una lolote la kumalizia?

Jibu; Kwa kumalizia, nataka kusema viongozi wachaguliwe kwa uadilifu, kwasababu ukiwachagua mafisadi, Mungu ataheshimu uteuzi wako, hatabadili kitu chochote!

Andrew Nyerere anaweza kupatikana kwa namba 0718- 536281, ikiwa unataka kuwasiliana na Nova Kambota mwandishi aliyefanya mahojiano haya piga simu namba 0712-544237, barua pepe; novakambota@gmail.com au tembelea http://novakambota.wordpress.com

 

Yote Uliyowahi Kutaka Kujua Kuhusu Mkito.com: Mahojiano Na Mwanzilishi Mwenza,Sune Mushendwa

$
0
0
Sune Mushendwa-Mkito.com

Sune Mushendwa

Kwa miaka nenda rudi, wasanii wa kitanzania walikuwa na kilio kinachofanana. Ungekaa pembeni bila kuwaona, ungedhani kutokana na mwangwi wa kilio chao, anayelia ni mmoja. Hapana. Wote walikuwa [na pengine bado wanaendelea kulia] kutokana na kunyonywa “jasho lao”.

Kimsingi “jasho” wanalolilia limekuwa ni soko na usambazaji. Kipaji unacho na watu wanakubali kazi zako. Tatizo utaifikishaje kazi yako kwa mashabiki zako? Ni wazi kwamba unahitaji msaada wa kimasoko na usambazaji. Kusema utaweza kufanya kila kitu peke yako ni kujidanganya.Nani? Yupo wapi na utampa kazi zako kwa thamani gani? Kilio chao kilianzia hapo. Wengine wakaamua kuachana na muziki [wengine muziki umewaacha wao] kutokana na ukosefu wa soko la uhakika na kuona kadhaa ya kupanga foleni ukisubiri “hela yako”.

Mabadiliko ya masoko ya kazi za wasanii duniani kutoka kwenye mifumo ya ki-analojia kwenda kwenye dijitali na pia kutoka katika mifumo ya vitu kama CD mpaka kwenda kwenye matumizi ya simu na vikabrasha vingine vya mikononi, kulimaanisha kwamba soko la wasanii wa kitanzania [na Afrika kwa upana wake] lilikuwa linazidi kufifia. Hakuna tena shabiki anayetaka kubeba furushi la CD. Inakuwaje?

Hapo ndipo baadhi ya vijana wakaona fursa kuthibitisha kwamba penye tatizo ndipo pa kukimbilia.Fursa ni kama dhahabu au almasi.Huwezi kuiokota kando ya bahari ikiwa imetupwa ufukweni na mawimbi ya bahari. Wazo la fursa likazaa Mkito.Com mahali ambapo wasanii sasa wanapumua na huku changamoto pekee ni kuwashawishi mashabiki kupakua kazi zao kutoka Mkito.Com. Kila mara shabiki anapofanya hivyo, msanii ananufaika na kupata nguvu zaidi ya kuingia tena studio kunogesha mambo. It’s a win win situation.

Sune Mushendwa [pichani juu] ni mwanzilishi-mwenza wa Mkito.Com. Kujua mengi zaidi nilimtafuta na kupiga naye story kidogo. Ameelezea mengi. Nakukaribisha usome mahojiano yangu naye ili ujue yote ambayo umekuwa ukitaka kuyajua kuhusu Mkito.Com .Twende pamoja;

BC: Sune karibu sana ndani ya BongoCelebrity. Hii ni mara yako ya kwanza hapa na bila shaka wasomaji wangependa kupata japo kwa kifupi tu historia yako. Ulizaliwa wapi,ukakulia wapi na kusomea wapi na mambo kama hayo?

SM: Asante sana kwa kunikaribisha. Mimi nimekulia Arusha na ndipo niliposoma pia. Baada ya sekondari nilienda kusoma chuo kikuu nchini Finland ambako mama yangu ndipo anapotokea.

BC: Wajasiriamali wengi ambao nimewahi kufanya nao mahojiano huniambia kwamba waliamua kufanya wanachokifanya baada ya kukosa au kubughudhiwa na kitu fulani.Huwa kuna kisa au mkasa nyuma ya pazia. Kwa upande wa Mkito kuna kisa au mkasa wowote? Ilikuwaje mpaka ukasema Aha…Mkito ikaanza? Na hili jina lilikuja namna gani?

SM: Baada ya kutoka masomoni nilianzisha studio ya muziki Arusha.Lakini tatizo kubwa lililoonekana moja kwa moja ni kwamba wasanii pamoja na studio zinapata tabu sana katika kusambaza na kuuza kazi zao. Niliona tunahitajika njia ya kuweza kusambaza muziki kirahisi na pia kuingiza kipato kwa msanii. Baada ya research na maandalizi ya zaidi ya miaka 4 ndipo Mkito.com ilipozaliwa tarehe 30 April 2014.

BC: Mpaka sasa Mkito imefanikiwa kuwa na wasanii wangapi? Nini masharti ya msanii kujiunga au kuweka kazi zake katika Mkito?

SM: Kuna wasanii takriban 600 waliojiunga mpaka sasa na wanaongezeka kila siku. Masharti ya kujiunga ni marahisi, uwe umerekodi wimbo anghalau mmoja wenye ubora. Baada ya hapo msanii anaweza kujitengenezea akaunti yake kupitia tovuti www.mkito.com na kupakia[upload] nyimbo zake mwenyewe. Msanii baada ya hapo anaweza kufuatilia mauzo yake mwenyewe kupitia akaunti yake aliyoitengeneza.

BC: Bado nikiwa katika swali au maswali ya wasanii. Msanii akishaingia katika mkataba au makubaliano na ninyi, bado anakuwa na haki na uhuru wa kuendelea kusambaza kazi zake katika platforms zingine kama vile iTunes,Spotify,Google Play nk?

SM: Tunaamini kuwa kazi ya msanii ni mali yake pekee kwahivyo hatumzuii msanii aliyejiunga nasi kusambaza kazi zake kwa njia yoyote nyingine aipendayo. Kama huduma yetu ni bora basi tunaimani msanii mweyewe atachagua kutumia huduma zetu siyo mpaka tumfunge kupitia mikataba.

BC: Nilisoma mahali kwamba mlipoanzisha Mkito lengo lilikuwa kuwa na watumiaji waliojiandikisha [registered users] milioni 1 katika mwaka wa kwanza. Mpaka sasa mmefikia wapi katika lengo hilo?

SM: Nilishasoma hilo mimi pia lakini siyo ukweli kuwa lengo ni kufikisha watumiaji milioni 1. Lengo ni kufikisha watumiaji waliyojiandikisha laki 5 ndani ya mwaka moja. Tumekaribia nusu ya hiyo idadi mpaka sasa na dalili zote ni kuwa tutafika na kuvuka hiyo idadi.

BC: Kuna baadhi ya wasanii ambao nimeongea nao kuhusu huduma kama hii ya Mkito na nyinginezo wanasema kwamba huduma hizi kimsingi zinawapunja au kuwadhulumu kwa sababu hamuendi nao bega kwa bega katika matayarisho ya muziki [kwa maana ya gharama na karaha zote za maandalizi] bali nyie mnasubiri wapike kisha muwasaidie tu kupakua huku nanyi mkijitengenezea faida. Unawaambiaje wasanii kama hao na kuna tofauti gani kubwa kati ya wasambazaji wale wa zamani na nyie hapo? 

SM: Mkito.com ni kampuni ya usambazaji wa muziki na siyo studio ya kurekodi au kampuni ya management. Kwa maana hiyo sisi faida tunaingiza katika uuzaji wa muziki kupitia tovuti yetu tu. Kama tungehusika na kurekodi na management ya wasanii basi tungedai makato kwenye mauzo yote kama ring tones, CD, shows n.k. lakini kama nilivyosema faida yetu ni katika uuzaji wa muziki tu.

Kuhusiana na tofauti ya Mkito.com na makampuni mengine; tangia mwanzo tumehakikisha kuwa mauzo yote yanawekwa wazi ili msanii ajue muda wote kuwa mauzo yake yakoje. Hili bado sijaona likifanyika na wengine ingawa ni la muhimu sana. Inabidi kujiuliza madhumuni ya haya makampuni kutokuweka mauzo wazi.

Mkito

BC: Kwa mtu ambaye hajui Mkito ni nini na angependa kufahamu zaidi na hata kujiunga na huduma ya Mkito[nazungumzia mtu mtumiaji wa kawaida] ungempa maelezo gani kwamba Mkito ni nini na nini ategemee pindi atakapoingia Mkito.com?

SM: Mkito.com ni huduma ya kwanza nchini ya kusambaza muziki kidigitali ambapo mtu anaweza kupakua nyimbo kwa sh 250 tu kupita simu yake au computer. Pia nyimbo zote zinapatikana bure lakini zinaambatanishwa na matangazo mafupi ya kibiashara. Haya matangazo katika nyimbo za bure ndiyo yanawalipa wasanii. Ni muhimu kujua kwa Watanzania wote kuwa ni jukumu letu kulinda muziki wetu na unavyopakua nyimbo kupitia Mkito.com unakuwa unauhakikia kuwa msanii analipwa kwa kazi yake na wewe pia unasaidia kuuendeleza muziki wa Kitanzania.

BC: Bila shaka kwenye biashara kama ya Mkito ambayo kwa ukaribu sana inahusiana na tekinolojia za mitandaoni,matatizo hujitokeza.Kuna mtu kushindwa kupakua[download] wimbo au nyimbo na kuna kero zingine nyingi.Mkito mnashughulikiaje matatizo kama hayo? Na kimsingi ni changamoto gani ambazo mnakabiliana nazo kila siku au mara kwa mara? 

SM: Kuna maelfu ya aina tofauti za simu na computer ambazo kila siku zinatumika kupakua nyimbo Mkito.com. Sasa ni vigumu kuhakikisha kuwa tovuti itafanya kazi na kila aina ya simu lakini kwa kiasi kikubwa sana tumefanikiwa kutatua matatizo yanapojitokeza. Pia tunayo huduma kwa wateja ili mtu akipata shida anaweza kutuandika barua pepe au kupiga simu na tunamsaidia kutatua tatizo lake haraka.

BC: Kwa upande wa muziki, wasanii,wasimamizi [managers] wao nk nikikupa nafasi hii kuongea nao moja kwa moja ungewaambia nini au ungewapa ushauri gani kuhusiana na suala zima la muziki nk?

SM: Muziki ni biashara, wote tunafahamu hilo. Kwahiyo ninawakaribisha wasanii wote kuja kujiunga Mkito.com tuwasaidie kutangaza, kusambaza na kuuza muziki wao. Nafahamu kuwa wengi wanakuwa na wasiwasi kuwa wataibiwa – hili siyo kweli kwa upande wa Mkito.com, labda waliotutangulia. Kama nilivyokwisha sema kila kitu kinawekwa wazi na kama wewe ni msanii mwenye kazi nzuri basi kuwa na imani kuwa unaweza kujipatia kipato kizuri kutokana na mauzo ya muziki wako kupitia Mkito.com

BC: Shukrani sana kwa muda wako Sune. Nakutakia kila la kheri katika kazi zako

Asante sana. Lakini na mimi nikuulize wewe swali moja. Je, umeshapakua nyimbo ngapi mpaka sasa kupitia Mkito.com ili kuwapa support wasanii wa Tanzania?

BC: Mpaka leo,nimeshapakua nyingi.Sikumbuki idadi kamili. Lakini mchango wangu zaidi ni kuwajulisha watumiaji wengine [wasomaji wangu kwa mfano] juu ya kazi mpya za wasanii na wapi pa kuzipata. Asante kwa swali zuri Sune.

Viewing all 48 articles
Browse latest View live


Latest Images